• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wananchi wa Ilkurot watakiwa kuacha kumbughudhi mwekezaji, umilki wa eneo lake ni halali

Posted on: August 31st, 2018

Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro, amewataka wananchi wa kijiji cha Engutukoit kata ya Oldonyowas, halmashauri ya Arusha, kuacha tabia ya kumzuia mwekezaji na mmiliki wa eneo lililopo kijijini hapo, kwa madai kuwa eneo hilo ni mali ya kijiji chao wakati sio kweli.

Mkuu huyo wa wilaya amewaonya wananchi hao, wakati wa mkutano wa kijiji hicho, ulioitishwa kwa lengo la kutoa kilio chao kwa mkuu huyo wa wilaya juu ya kuporwa ardhi yao na mwekezaji anayemiliki eneo hilo.

Hata hivyo baada ya mkuu huyo wa wilaya kusikiliza hoja za pande zote mbili, ilionekana mwekezaji huyo, ndio mwenye hati halali ya umiliki wa eneo hilo, baada ya watalamu wa ardhi kuthibitisha eneo hilo si mali ya kijiji bali ni mali halali ya mwekezaji huyo.

Ameongeza kuwa, wananchi wanapaswa kufuata sheria za nchi na kuwaonya kuwa kuvami eneo lolote ni kosa kisheria na kuwataka wananchi hao kuachana na tabia hiyo, badala yake kukaa pamoja na mwekezaji huyo kuona namna ya  wananchi wanawezaje kunufaika kupitia uwekezaji wake.

"Ninataka mtambue kuwa eneo hilo ni eneo halali la mwekezaji huyo na anavielelezo halali vya umiliki wa ardhi kisheria, sasa namuagiza Mwenyekiti wenu kutafuta watalamu wa kumwezesha, kutambua maeneo ya kijiji chenu na kufahamu mipaka yake kwa kua amekiri mbele yenu hafahamu maeneo ya kijiji" amesema Muro            

Amewasisitiza viongozi wa kijiji hicho kukaa na kuwaelimisha wananchi wao juu ya utii wa sheria za nchi pamoja na kukaa na mwekezaji huyo ili kupanga namna uwekezaji huo utakavyowaanufaisha wananchi wenu kupitia ardhi hiyo iliyo ndani ya kijiji choa.  

Awali akisoma taarifa na vielelezo vya uhalali wa  umiliki wa eneo hilo, Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili, halmashauri ya Arusha Khafti Tarimo, amesema kuwa, hati ya umiliki wa eneo hilo ilitolewa kwa mara ya kwanza mwa 1965 na ilikuwa ikimilikiwa na wananchi watano, ambao waliuza eneo hilo kwa kampuni ya JODISTA Ltd mwaka 1990 na baadaye, kampuni hiyo kumuuzia mwekezaji wa sasa na  hati hiyo kuhamishwa miliki yake mwaka 2012 kwa kufuata kanuni, sheria na taratibu halali za umiliki wa ardhi.

Hata hivyo katika hali isiyokuwa ya kawaida, wananchi wa kijiji cha Engutukoit wameibua mgogoro na mwekezaji huyo, kwa madai kuwa eneo hilo ni mali ya kijiji chao na kuzumzuia mwekezaji huyo kufanya shughuli yoyote ya kuendekeza eneo hilo na kufikia hatua ya kuwazuia hata watalamu wa halmashauri kufika katika eneo hilo.

Aidha serikali inawataka viongozi wote wa vijiji, kutambua mipaka ya vijiji vyao ikiwa ni pamoja na kuwatambua wamiliki halali wa maeneo yaliyo ndani ya vijiji vyao, sambamba na kufahamu mipango wa matumizi ya maeneo hayo ili kuepuka migogoro isiyo ya lazima baina ya wananchi na wamiliki wa maeneo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.