• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wananchi wa kijiji cha Lesiraa, kata ya Kisongo, wamemuomba Naibu Waziri wa Afya, kusaidia ukarabati wa Zahanati yao

Posted on: June 9th, 2020

Na. Elinipa Lupembe.

Wananchi wa kijiji cha Lesiraa kata ya Kisongo, halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru, wamemuomba Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Godwin Mollel, kuwasaidi kufanya ukarabati wa jengo la zahanati ya kijiji hicho, jengo ambalo limekuwa chakavu,kutokana na kujengwa muda mrefu sasa.

Wananchi hao wametoa kilio chao, wakati Naibu waziri huyo, alipotembelea zahanati hiyo, wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Arusha, ya kukagua miradi ya afya, utoaji na upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi wa maeneo ya vijijini.

Akizungumza mbele ya Naibu waziri, Mwenyekiti wa kijiji cha Lesiraa, Injinia Sakaya, amesema kuwa, jengo la zahanati hiyo, lilijengwa na wananchi mwaka 2010 na kwa sasa limekuwa na nyufa nyingi, kiasi cha kutishia usalama wa wauguzi na wagonjwa kwa kuhofia jengo hilo kuangua.

Amemuomba Naibu Waziri, kuangalia tatizo lao kwa jicho jingine, kutokana na umuhimu wa upatikanaji huduma ya afya kwa karibu,kutokana ukweli kuwa, zahanati hiyo inahudumia zaidi ya wananchi 2000, huku kukiwa, hakuna huduma za afya jirani, jambo ambalo huwalazimu kwenda haspital ya Jeshi Monduli au Kisongo umbali wa zaidi ya Kilomita 16 kwenda na kurudi.

Saitoti Lemilya, mkazi wa kijiji cha lesiraa, ameweka wazi kuwa, licha ya uchakavu wa jengo hilo, jengo hilo halina umeme pamoja na miundombinu mibovu ya barabara ya kufika kituoni hapo, hasa kipindi cha mvua.

"Nguzo za umeme zimewekwa tangu mwaka 2012, hakuna mwananchibaliyeunganishiwa umeme, mheshimiwa tusaidie tupate umeme ili kuboresha huduma za afya kwenye zahanati yetu" amesema Lemilya.

Naye Monica Saruni, amesisitiza kuwa, kina mama wajawazito wanateseka wakati wa kujifungua, hasa nyakati za usiku, muuguzi hutumia tochi kuwazalisha jambo ambalo, huhatarisha maisha ya mama na mtoto wakati wa kujifungua.

"Tunahitaji umeme ili kina mama waweze kujifungua kwa usalama, lakini pia utawezesga kupata huduma za maabara" amesema Monica.

Hata hivyo Naibu Waziri huyo, amewaahidi wananchi hao, kushughulika matatizo hayo na kufafanua kuwa, lengo la serikali ni kufikisha huduma za jamii hasa za afya karibu na wananchi, hivyo ni haki yao kupata huduma hizo na kuwataka wananchi wa Lesiraa, kuwa wavumilivu wakati serikali ikijipanga kutatua matatizo yao.

Aidha amewapongeza wananchi hao kwa kujenga zahanati hiyo, huku akiwapongeza wahudumu wa afya wa zahanati hiyo, licha ya uchakavu wa majengo lakini zahanati ni safi, vifaa vimepangiliwa vizuri  na inaendelea kuwahudumia wananchi.

"Nimejionea hali halisi, lakini  niwatie moyo wananchi, mkakati wa serikali ya awamu ya tano ni kusogeza huduma za jamii kwa wananchi hasa waishio vijijini, mwananchi apate huduma muhimu ndani ya kijiji chake, tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa, lakini kuweni wavumilivu, tatizo hili litakwenda kumalizika kwa ushirikiano wenu wananchi na serikali yenu makini"amesisitiza Naibu Waziri huyo.








K


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.