• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wananchi wa kijiji cha Midawe kata ya Bangata wajengewa zahanati

Posted on: June 17th, 2018

Wananchi wa kijiji cha Midawe, kata ya Bangata, halmashauri ya Arusha, kupitia uongizi wa awamu hii ya tano, wamekuwa na matumaini ya kufikiwa na huduma za afya kijijini kwao, huduma ambayo haikuwahi kuwepo zaidi ya miaka hamsini na tano, tangu kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika.

Matumaini hayo yamekuja, baada ya wananchi wa kijiji hicho kuamua kutoa eneo kwa ajili ya kujenga zahanati ya umma kwa wananchi wa kijiji hicho, kupitia mradi wa TASAF awamu ya III na tayari ujenzi wa zahanati kijijini hapo umeshaanza.

Wakizungumza na mwandishi wetu, alipotembelea eneo inapojengwa zahanati hiyo, wananchi hao wamekiri wazi kuwa, ujenzi huo wa zahanati umekuja wakati muafaka kutokana na adha wanayoipata ya kulazimika kutembea Kilomita tatu, kwenda kutibiwa kwenye kijiji cha jirani, hospitali ya West Meru na hospitali ya wilaya iliyo umbali wa kati ya  kilomita kumi na kumi na mbili.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi ya Zahanati hiyo Loirai Ndossi, amethibitidha kuwa, kijiji hicho hakijawahi kuwa na zahanati tangu kupatikana kwa uhuru, na kuongeza kuwa uwepo wa zahanati hiyo, licha ya kuwapunguzia gharama za kutafuta huduma za afya lakini pia itapunguza vifo vya kina mama na watoto ambavyo, hutokea kutokana na kuchelewa kupata huduma.

Ameongeza kuwa kutokana na adha kubwa wanayoipata, baadhi ya wananchi wa Midawe, wakaamua kutoa eneo hili kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati hii na eneo jingine kwa ajili ya kujenga nyumba ya mtumishi wa afya.

Ester Elisha anasema kuwa, ukosefu wa zahanati kijijini kwao unasababisha kusuasua kwa baadhi ya kina mama wajawazito kushindwa kuhudhuria kliniki kwa utaratibu kutokana na umbali, jambo linalosababishwa wengine kulazimika kujifungulia nyumba au kwa wakunga wa jadi, na kuhatarisha maisha na afya ya mama na mtoto.

"Hapa kijijini baadhi wajawazito wanashindwa kuhudhuria kliniki kwa utaratibu unaofaa, kutokana na umbali na wengine kuamua kujifungulia nyumbani, mama anapata uchungu, hana hela ya kwenda hospitali Patandi au Mount Meru, analazimika kujifungua nyumbani" amesema Ester.

Alex Ngira mkazi wa Midawe ameelezea kuwa wakati mwingine, wananchi hushindwa kumudu gharama za usafiri na matibabu na kulazika kununua dawa dukani bila hata ya kupima.

 "Ukingalia hela uliyonayo ni ya dawa tuu, huna nauli unaona bora nikanunue dawa nimeze, Mungu akijalia ukipona basi lakini wengine hujikuta wanapata madhara makubwa kwa kunywa dawa bila kupima" amesema Ngira.

Ndeelo Nyari amefafanua zaidi kuwa, ujenzi wa zahanati hiyo ya Midawe ni neema kwa wananchi kijijini hapo kwani wamechoka kutmbea umbali mrefu kutafuta huduma za afya na wakati mwingini watu hupoteza maisha.

"Hapa kijijini kama unavyoona ni mbali, mtu akiugua tunambeba na machela mpaka barabarani, tumepoteza wapendwa wetu sana kutokana na kijiji hiki kukosa zahanati". Amesema Nyari

Mratibu wa TASAF halmashauri ya Arusha, Grace Makema amesema kuwa, mradi huo wa zahanati umetengewa  shilingi miloni 70.1 na unategemea kukamilika mwishoni mwa mwaka huu 2018.

Makema ameongeza kuwa, miradi hii inayotekelezwa na TASAF awamu ya tatu, huibuliwa na wananchi wenyewe kulingana na uhitaji na vipaumbele vyao wenyewe katika maeneo yao.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.