• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WA LAROI WAACHANA NA KERO YA KORONGO, BAADA YA UJENZI WA DARAJA KUKAMILIKA

Posted on: August 20th, 2020

Na. Elinipa Lupembe.

     Wananchi wa kijiji cha Laroi, halmashauri ya Arusha, wameondokana na kero kubwa ya ukosefu wa kivuko, iliyokuwa ikiwatesa kwa kipindi chote cha maisha yao, kero iliyomalizika baada ya kukamilika kwa ujenzi wa daraja, mradi uliotekelezwa na serikali kupitia miradi ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF awamu ya III, kupitia miradi yake ya OPEC III.

        Wananchi hao, wemethibitisha hayo wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa mradi huo na serikali ya mkoa wa Arusha kwa kushirikia na halmashauri ya Arusha, baada ya kukamilika,  hafla iliyofanyika kijijini hapo na kusababisha nderemo na vifijo vya wanawake wa kijiji hicho, muda wote wakati wa makabidhiano.

      Wamesema kuwa, kukamilika kwa mradi huo wa ujenzi wa daraja, umeleta faraja na matumaini makubwa kwa wananchi wa kijiji cha Laroi, hasa wanawake wajawazito na watoto, walioteseka kuvuka korongo hilo, wakati wa msimu wa mvua, korongo hilo likiwa limejaa maji na wakati mwingine kusababisha vifo vya wapendwa wao, watu kushindwa kitoka au kurudi nyumbani na watoto kushindwa kwenda shule au kurudi nyumbani baaa ya masomo.

     Ester Lobulu, mkazi wa Laroi, amesema kuwa licha ya daraja hilo kurahisisha mawasilino ya kijiji hicho lakini pia litaokoa maisha ya watu kwa kuwa, kwa kipindi cha mvua, ndugu zao walikuwa wakipoteza maisha kwa kusombwa na maji, jambo ambalo liliwatia simanzi kubwa sana kila unapofika msimu wa mvua

     "Tunaishukuru serikali na TASAF kwa kutusaidia daraja, tulikuwa tumekata tamaa, na wakati mwingine tunaichukia mvua, kwani kipindi cha mvua mawasiliano yalikatika ndani ya kijiji, na ndugu zetu walikufa, kwa sasa tunanamini watu wa Laroi hawatakufa tena" amesema Ester.

       Hata hivyo, wananchi hao wa Laroi, licha ya kuishukuru serikali ya awamu ya tano, wamemuomba Rais Magufuli kuwasaidia ujenzi wa kituo cha afya, kwani kina mama wajawazito huteseka kwa kufuata huduma za afya umbali wa zaidi ya Kilomita 20 na kusababisha matatizo kwa wajawazito na watoto.

     "Tunashukuru kwa daraja, kwa sasa tunapita kwa raha, watoto wetu wanakwenda shule kwa amani, lakini Baba yetu Magufuli, tunaomba usikie kilio chetu, kina mama wanajifungulia njia, huku Laroi hatuna hospitali, tunamuomba atusaidie kama alivyotusaidia daraja" amesisitiza mama Vicktoria Olais.

    Awali kabla ya kukabidhi mradi huo, mgeni rasmi na Mratibu wa TASAF mkoa wa Arusha Seif Mathias, amewataka wananchi hao, kulitunza daraja hilo na kuhakikisha kila mmoja anakuwa mlinzi wa mwenzake pamoja na kuzuia kupita magari yenye uzito uliozidi uwezo wa daraja hilo, uzito wa tani 10 na si vinginevyo.

       "Daraja hili ni lenu, serikali imemaliza jukumu lake, kazi yenu kubwa ni kulitumia na kulitunza, mhandisi amesema daraja linaruhusu kupita gari yenye tani 10, msiruhusu magari yenye mzigo wa zaidi ya tani hizo,  ili daraja hilo lidumu na litumike kwa vizazi na vizazi, laiki pia hakikisheni mnatunza mazingira kwa kuanza kupanda miti na mikonge kuzuia mmomonyoko" amesema Mathias .

       Ujenzi wa daraja hilo, umekamilika kwa ushirikiano wa Serikali na wananchi kwa gharama ya  shilingi milioni 88.8, ikiwa  TASAF ilitoa shilingi milioni 73, Halmashauri shilingi milioni 6.4 na wananchi wa Laroi walichangia nguvu kazi iliyothaminishwa kwa shilingi milioni 9.3.


PICHA ZA MATUKIO

Mratibu wa TASAF mkoa wa Arusha  Mathias  akukata utepe kufungua Daraja la Laroi.








Matangazo

  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA TATU 2O21/2022 tarehe 09.05.2022 May 08, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA ARUSHA DC,BW.SELEMAN MSUMI AKIWA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI HIYO KATIKA MASDHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA ARUSHA

    May 02, 2025
  • HERI YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • HERI YA SIKU YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • MHE. MAJALIWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.