Na Elinipa Lupembe
Wananchi wa kijiji cha Lemanda kata ya Oldonyosambu wameishukuru serikali kwa kupata mradi mkubwa wa ujenzi wa shule mpya ya msingi.
Wananchi hao wametoa shukurani zao walipojitokeza kuchimba msingi wa majengo wakati wa uzinduzi ujenzi wa majengo ya shule hiyo, uliofanyika mapema jana.
Diwani wa kata ya Oldonyosambu, Mhe. Raymond Lairumbe, ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuketa mradi mkubwa kata hiyo, mradi ambao unakwenda kutimiza ndoto za watoto wa jamii ya wafugaji kwenda shule.
Ameeleza kuwa uwepo wa shule hiyo, licha ya kupunguza adha ya watoto kutembea umbali wa zaidi ya Km 20, kwenda na kurudi shuleni itasaidia watoto wengi wa eneo hilo kupata elimu kama ilivyo haki ya mtoto wa kitanzania.
"Shule hii tumeipa jina la Naisula, ikimaanisha ushindi uliopitiliza, hakika kuwepo kwa shule hii ni ushindi kwa watoto wa Lemanda na jamii nzima ya wafugaji, watoyo ambao walishindwa kupata fursa ya kupata elimu kutokana na umbali mrefu" Amefafanua Mhe. Lairumbe
"Kina mama wa Lemanda, tumefuhi sana kujengewa shule hapa kijijini, watoto wetu waliteseka kutembea umbali mrefu, hata sisi wazazi hatukuwa na amani pale watoto walipokwenda shuleni mbali hasa kipindi cha mvua, kwa ukaribu huu wa shule, tutakuwa na amani na watoto watafurahi, tunamshukuru Mama Samia ametujali wakina mama wa Lemanda" Amefafanua Esuvat Jackson
Seuri Lesuroi, amesema kuwa hata yeye hakupata fursa ya kusoma jambo ambalo linamuuma sana, na kuongeza kuwa hata watoto wengi wa kike hukatiza masomo na kuolewa kutokana na fursa finyu za upatikanaji wa elimu karibu
"Uwepo wa shule hapa kijijini, tunaamini watoto wote watakwenda shule na kutimiza ndoto zao, ndoa za utotoni kwa sasa zitaondoka kwa watoto wetu".Amesisitiza Lesuroi.
Naye Mwenyekiti wa CCM kata ya Oldonyosambu, ameishukuru serikali kwa utekelezaji wa Ilani ya Chama kwa vitendo Joseph Saria, watoto wetu wa kimasaai nao watasoma kama watoto wengine, wasichana wataacha kuolewa na vijana wa kiume kukimbilia Nairobi kufanya kazi za ulinzi.
Hata hivyo mchungaji wa Kanisa la Kiinijili la Kilutheri Usharika wa Oldonyosambum Mchg. Daniel Ole Kambaine, licha ya kuombea eneo hilo la ujenzi, ameishukuru serikali kwa neema hiyo iliyowashukia watoto wa Lemanda, neema ambayo wanaamini itawapa watoto hao kupata elimu itakayowasaidia kujitawala katika shughuli zao za kila siku.
Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Lemanda, kwa niaba ya wananchi wake, wameahidi kushirikiana na watalamu na mafunzi kusimamia hatua zote za utekelzaji wa mradi huo mpaka utakapokamilika na watoto wao kuanza masomo.
Awali Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI imetoa fedha kiasi cha shilingi milioni 306.5 kwa ajli ya ujenzi wa shule mpya ya msingi, huku kiasi hicho cha fedha kitajumuisha ujenzi wa vyumba 9 vya madarasa, jengo la Utawala pamoja na matundu 16 ya vyoo, ikiwa ni madarasa mawili kati ya hayo, yakiwa ni maalum kwa wanafunzi wa elimu ya awali na madarasa 7 ya shule ya msingi.
Ikumbukwe kuwa, jumla shilingi milioni 682.5 zimetolewa na serikali kuu, fedha za ujenzi wa miundombinu ya shule kwa shule 6 za msingi halmasahuri ya Arusha.
Ikumbukwe kuwa, miradi hiyo ya ujenzi wa miundombinu shule za msingi ni utekelzaji wa Ilani ya CCM, Sura ya tatu Ibara ya 79 kifungu (q)Kukarabati miundombinu ya kufundishia na kujifunzia na kifungu (C)Kuboresha uratibu na usimamiaji wa stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu.
ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.