• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WA LEMANDA WAISHUKURU SERIKALI KUPATA MILIONI 306.9 ZA UJENZI WA SHULE MPYA YA MSINGI KUPITIA MRADI WA BOOST

Posted on: May 17th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Wananchi wa kijiji cha Lemanda kata ya Oldonyosambu wameishukuru serikali kwa kupata mradi mkubwa wa ujenzi wa shule mpya ya msingi.


Wananchi hao wametoa shukurani zao walipojitokeza kuchimba msingi wa majengo wakati wa uzinduzi ujenzi wa majengo ya shule hiyo, uliofanyika mapema jana.


Diwani wa kata ya Oldonyosambu, Mhe. Raymond Lairumbe, ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuketa mradi mkubwa kata hiyo, mradi ambao unakwenda kutimiza ndoto za watoto wa jamii ya wafugaji kwenda shule.


Ameeleza kuwa uwepo wa shule hiyo, licha ya kupunguza adha ya watoto kutembea umbali wa zaidi ya Km 20, kwenda na kurudi shuleni itasaidia watoto wengi wa eneo hilo kupata elimu kama ilivyo haki ya mtoto wa kitanzania.


"Shule hii tumeipa jina la Naisula, ikimaanisha ushindi uliopitiliza, hakika kuwepo kwa shule hii ni ushindi kwa watoto wa Lemanda na jamii nzima ya wafugaji, watoyo ambao walishindwa kupata fursa ya kupata elimu kutokana na umbali mrefu" Amefafanua Mhe. Lairumbe


"Kina mama wa Lemanda, tumefuhi sana kujengewa shule hapa kijijini, watoto wetu waliteseka kutembea umbali mrefu, hata sisi wazazi hatukuwa na amani pale watoto walipokwenda shuleni mbali hasa kipindi cha mvua, kwa ukaribu huu wa shule, tutakuwa na amani na watoto watafurahi, tunamshukuru Mama Samia ametujali wakina mama wa Lemanda" Amefafanua Esuvat Jackson


Seuri Lesuroi, amesema kuwa hata yeye hakupata fursa ya kusoma jambo ambalo linamuuma sana, na kuongeza kuwa hata watoto wengi wa kike hukatiza masomo na kuolewa kutokana na fursa finyu za upatikanaji wa elimu karibu


"Uwepo wa shule hapa kijijini, tunaamini watoto wote watakwenda shule na kutimiza ndoto zao, ndoa za utotoni kwa sasa zitaondoka kwa watoto wetu".Amesisitiza Lesuroi.


Naye Mwenyekiti wa CCM kata ya Oldonyosambu, ameishukuru serikali kwa utekelezaji wa Ilani ya Chama kwa vitendo Joseph Saria, watoto wetu wa kimasaai nao watasoma kama watoto wengine, wasichana wataacha kuolewa na vijana wa kiume kukimbilia Nairobi kufanya kazi za ulinzi.


Hata hivyo mchungaji wa Kanisa la Kiinijili la Kilutheri Usharika wa Oldonyosambum Mchg. Daniel Ole Kambaine, licha ya kuombea eneo hilo la ujenzi, ameishukuru serikali kwa neema hiyo iliyowashukia watoto wa Lemanda, neema ambayo wanaamini itawapa watoto hao kupata elimu itakayowasaidia kujitawala katika shughuli zao za kila siku.


Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Lemanda, kwa niaba ya wananchi wake, wameahidi kushirikiana na watalamu na mafunzi kusimamia hatua zote za utekelzaji wa mradi huo mpaka utakapokamilika na watoto wao kuanza masomo.

Awali Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI imetoa fedha kiasi cha shilingi milioni 306.5 kwa ajli ya ujenzi wa shule mpya ya msingi, huku kiasi hicho cha fedha kitajumuisha ujenzi wa vyumba 9 vya madarasa, jengo la Utawala pamoja na matundu 16 ya vyoo, ikiwa  ni madarasa mawili kati ya hayo, yakiwa ni maalum kwa wanafunzi wa elimu ya  awali na madarasa 7 ya shule ya msingi.


Ikumbukwe kuwa, jumla shilingi milioni 682.5 zimetolewa na serikali kuu, fedha za ujenzi wa miundombinu ya shule kwa shule 6 za msingi halmasahuri ya Arusha.


Ikumbukwe kuwa, miradi hiyo ya ujenzi wa miundombinu shule za msingi ni utekelzaji wa Ilani ya CCM, Sura ya tatu Ibara ya 79 kifungu (q)Kukarabati miundombinu ya kufundishia na kujifunzia na kifungu (C)Kuboresha uratibu na usimamiaji wa stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu.

ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.