Na Elinipa Lupembe
Wahasibu na watumishi wanaohusika na masuala ya fedha kwenye Hospitali, vituo vya afya, zahanati, shuke za msingi na sekondari pamoja na vijiji na kata halmaahauri ya Arusha wametakiwa kuhakikisha wanatumia vema mfumo wa malipo ya Serikali (Facilty Financial Account and Reporting System ( FFARS) ili kufikia lengo la serikali la matumizi sahihi na salama ya fedha za Umma.
Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Kitengo cha Fedha, halmashauri ya Arusha CPA David Rubibira wakati akifungua mafunzo ya siku 5 yatakayowajengea uwezo wahasibu na watunza fedha za serikali wa kutumia mfumo huo wa FFARS awamu ya pili, mafunzo yanayoendelea kwenye ukumbi mdogo wa halamashauri ya Arusha.
Licha ya kuwataka kuwa makini wakati wa mafunzo hayo, amesisitiza kwenda kutumia vema mfumo huo wa FFARS unawezesha kuwepo na uwazi na uwajibikaji sehemu za kutolea huduma hususani kwenye mashule na vituo vya kutolea huduma za afya na utasaidia ufuatiliaji wa matumizi sahihi ya fedha zinazoingizwa kwenye akaunti zote za Umma.
"Mfumo huu pia utawezesha fedha zitumike kulingana na bajeti iliyopitishwa pamoja na upatikanaji wa taarifa mbalimbali kutoka kwenye vituo vya kutolea huduma ikiwemo taarifa za mapato ya kila mwezi, hivyo mkiutumia vizuri utawarahisishia kazi na kutuondela hoja za ukaguzi zisizo za lazima" Amefafanua CPA. Rubibira
Ameongeza kuwa FFARS imeunganishwa na mifumo mingine ya serikali ikiwemo mfumo wa PlanRep unaoandaa na kutoa taarifa za utekelezaji wa bajeti pamoja na kuonesha mapokezi ya fedha na fedha zilizoingia benki.
Naye mratibu na mwezeshaji wa Mafunzo ya Mfumo huo wa FFARS halmashauri ya Arusha Joseph Chenya, amesema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa watumishi wote wanaohusika na mifumo ya fedha za serikali na yatafanyika kwa awamu tatu tofauti ili kuwapa furasa watumishi hao kupata uwelewa wa pamoja juu ya matumizi sahihi ya mfumo huo.
Amesema kuwa wameanza na Wahasibu na walimu wa fedha kwa shule za sekondari, na kufuatia walimu wa fedha shule za msingi, wahasibu wa vituo vya afya na zahanati na kumalizia kwa Maafisa Watendaji wa vijiji na kata.
ARUSHA DC NI YETU, TUSHIRIKIANE KUIJENGA ✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.