Na Elinipa Lupembe
Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani tarehe 08. Machi, Wanawake wameshauriwa kusajili vikundi vya huduma ndogo za fedha maarufu kama 'VICOBA' ili vitambulika kisheria kwa usalama wa fedha wanazowekeza na kukopeshana lengo likiwa kuepuka kutapeliwa.
Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, halmashauri ya Arusha, Stedvant Kileo, wakati wanawake wa kata ya Kiutu, wakiadhimisho ya siku ya wanawake Duniani, sherehe zilizofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Sekei.
Amesema kuwa wanawake wengi hupoteza pesa zao kwa kukopeshana kwenye vikundi visivyo sajiliwa na kushindwa kupata msaada wa kisheria pindi wanapopata changamoto za kutapeliwa na wanavikundi wenzao na kusababisha kushindwa kuchukuliwa hatua zozote, kutokana na vikundi hivyo kutokusajiliwa na kutambulika kisheria.
Hata hivyo Kileo amebainisha kuwa serikali baada ya kugundua changamoto hiyo, bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limetinga sheria ya kusimamia vikundi vya kijamii vya huduama ndogo za fedha (VICOBA) kwa visajili bure kwenye halmashauri husika ili vitambulike kisheria.
"Uzoefu unaonesha, kutokana baadhi ya vikundi kufanyashughuli za kuweka na kukopa bila kusajiliwa, vikundi vimepoteza fedha kwa kudhulumiwa na wanavikundi wenzao, huku serikali ikishindwa kuwabana watuhumiwa hao, sajilini bikundi ili kuepukana na hasara hizo". Amefafanua Kileo.
Hata hivyo Kileo amewasisitiza wanawake wenye vikundi vya VICOBA, kufika ofisi za makao makuu ya halmashauri kupata msaada wa namna ya kusajili vikundi na kuwathibitishia kuwa vikundi hivyo kwa sasa vinasajiliwa bure bila malipo.
Siku ya Wanawake Duniani huadhimishwa tarehe 08.Machi kila mwaka, kina mama wa kata ya Kiutu wameadhimisha siku hiyo muhimu kwa yenye Kauli mbiu isemayo "Ubunifu na Mabadiliko ya Teknolojia: Chachu katika kuleta Usaw wa Kijinsia"
"ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"
#kaziinaendelea✍✍✍✍
PICHA ZA MATUKIO
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.