• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANAWAKE NA VIJANA  CHANGAMKIENI FURSA ZA KILIMO , MIFUGO NA UVUVI ZINAZOANDALIWA NA SERIKALI

Posted on: August 3rd, 2023


Na. Elinipa Lupembe

Wanawake na vijana wamehimizwa kuona umuhimu na kuhakikisa wanachangamkia fursa wanazoandaliwa na serikali kwenye sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa kuwa wao ndio msingi wa maendeleo na mabadiliko katika sekta hiyo.

Rai hiyo imetolewa na
Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zubeir Maulid, wakati akifungua maonesho ya Nanenane kuelekea maadhimisho ya sherehe za Wakulima na Wafugaji Kanda ya Kaskazini, yanayoendelea kwenye viwanja vya Themi - Njiro mkoani Arusha 

Amesema serikali imeona umuhimu wa wanawake na vijana katika sekta ya Kilimo hususani katika msingi imara wa mifumo ya chakula kuanzia shambani, sokoni mpaka kumfikia mlaji bila kikiwa salama kwa afya na kuwasisitiza kuchangamkia fursa hiyo.

"Licha ya changamoto zinazowakabili wakulima,  sekta ya Kilimo, Uvuvi na Ufugaji imekuwa na mchango mkubwa katika taifa, hivyo  maonesho ya Nanenane yatumike kuhakikisha teknolojia za Kilimo, Uvuvi na Ufugaji zinawafikia wananchi hususani katika kuongeza mnyororo wa thamani ili kuongeza zaidi fursa za upatikanaji wa chakula na kujenga uchumi wa mtu mmoja"Amebainisha Mhe. Spika

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella ameweka wazi kuwa, zaidi ya  asilimia 60 ya watanzania wapo kwenye sekta ya kilimo wakijishughulisha na kilimo, ufugaji na uvuvi hivyo maonesho ya Nanenane ni chachu ya maendeleo kwa wakulima na huchochea uchumi wa wakulima na maendeleo ya Taifa kwa zujumla wake.

Mhe. Mongela amefafanua kuwa maonesho hayo yanazidi kuimarika mwaka hadi mwaka huku yakileta tija kwa wananchi na wakulima kwa kupata fursa  elimu, ushauri wa matumizi ya teknolojia mbalimbali rahisi na za kisasa kurahisisha kilimo pamoja na upatikanaji wa masoko.

"Licha ya kuwaonesha teknolojia za kisasa za Kilimo na Ufugaji, maonesha ya Nanenane yanaendelea kuwa chachu ya mabadilika katika sekta hiyo pamoja na kuwaunganisha wakulima na wataalamu wa sekta hiyo na masoko ya mazao yao" Amesema Mkuu huyo wa mkoa

Akizungumza kwaniaba ya wakuu wa Mikoa ya Manyara na Kilimanjaro, Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga, amesema kuwa lengo la maonesho hayo ya Nanenane nikutoa elimu mubashara kwa njia ya kuona na kubadilishana uzoefu kwa wakulima na wafugaji wa mikao hiyo mitatu ili kupata uzoefu na kufanya kilimo cha kisasa chenye tija kwa wakulima na taifa.

Awali Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Nanenane, Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Missaile Musa amesema kuwa, maandalizi yalianza mwezi Aprili kwa kuandaa vitalu katika maeneno tofautitofauti na hatimaye kuanza rasmi tarehe 01.08.2023 yakihusisha wakulima, wafugaji, wavuvi, taasisi na makapuni ya kilimo pamoja na wadau wa sekta ya kilimo kutoka mikoa mitatu ya Kanda ya Kaskazini.

Maonesho ya nanenane Kanda ya Kaskazini  2023a mefunguliwa rasmi Agosti  3, yenye kauli mbiu ya  "Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mifumo ya chakula", na yanatarajiwa kufungwa mapema Agosti 8, 2023.




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.