• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wanawake wachangamkia fursa ya uanzishaji viwanda

Posted on: March 9th, 2018

Wanawake wajasiriamali halmashauri ya Arusha wilayani Arumeru wamechangamkia fursa ya uanzishaji wa viwanda tangu serikali ya awamu ya tano kutangaza kutekeleza  sera ya viwanda kuelekea uchumi wa kati.         Hali hii imeonekana baada ya tafiti kuonesha kuwa karibu asilimia 60% ya Wanawake wajasiriamali wamejikita kwenye  biashara ya usindikaji na utengenezaji wa bidhaa mbalimbali shughuli wanazozifanya ndani ya nyumba zao ambazo kiuhalisia ni shughuli za viwanda vidogo.       
    Awali wanawake hao walikuwa wakifanya shughuli hizo bila kutambua kuwa uzalishaji wa bidhaa hizo ni viwanda vidogo mpaka hapo halmashauri kupitia Idara ya maendleo ya Jamii na Kitengo cha Biashara kuainisha na kuzitambua shughuli hizo kama viwanda vidogo.
      Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya ofisi za makao makuu halmashauri ya Arusha mgeni rasmi mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Dkt. Wilson Mahera amesema kuwa karibu asilimia  60% ya wanawake wajasiriamali wamejikita kwenye shughuli za uzalishaji wa malighafi na bidhaa za viwanda katika halmashauri hiyo. 
       Mkurugenzi Mahera ameongeza kuwa kuelekea uchumi wa viwanda Wanawake wamonesha  kuwa suluhisho la uanzishaji wa viwanda katika halmashauri hiyo na kuahidi kuendelea kuwasimamia ili viwanda hivyo vidogo kuwa vya kati mpaka vikubwa.    
 "Tutahakikisha viwanda hivi vinakua na kuwa viwanda vikubwa kwa kuwawezesha kuongeza mitaji, kusajili na kupata vibali vyote pamoja na kuwaunganisha na maeneo ya masoko ndani na nje ya nchi" amesema Mkurugenzi Mahera.              Wakizungumza wakati wa maonesho ya bidhaa, wanawake hao wamedhihirisha kuwa,    licha ya kumiliki kwao viwanda vidogo bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo mitaji ya kuendesha uzalishaji, usajili wa bidhaa zao pamoja na masoko ya kuuzia bidhaa zao kutokana na ushindani wa soko la bidhaa kutoka nje ya nchi.                    Joyce Mollel mwanamke anayejishughulisha na utengenezaji wa dawa za kusafishia vioo, amesema kuwa mtaji kwao ni tatizo  jambo ambalo linasababisha uzalishaji kuwa wa kiwango cha chini ukilinganisha na uhitaji wa bidhaa sokoni.         " Bidhaa zetu zinasoko kubwa ndani na nje ya nchi, tupepata soko nchini Kenya, mtaji wetu ni mdogo kiasi cha kushinda kukidhi uhitaji wa bidhaa sokoni" amesema Joyce              Wanawake hao pia wamelalamikia kasumba ya watanzania kupenda kununua bidhaa kutoka nje ya nchi na kudharau bidhaa zinazotengenezwa  nchini na watanzania wenzao na kuwataka watanzania kufuta kasumba hiyo badala yake kuwa wazalendo kwa kununua bidhaa za nyumbani ili kukuza uchumi wa nchi yao.                    Hata hivyo mkurugenzi Mahera amewahakikishia wanawake hao kuweka juhudi katika ukukusanyaji wa mapa ili kuendelea kutoa mikopo ya wanawake kupitia asilimia 4%    za mapato hayo pamoja na kuwajengea uwezo wa kuweka na kukopa na kuwaunganisha na taasisi za fedha zinazotoa mikopo ya wajasiriamali kwa riba nafuu kwa wale wanaohitaji mitaji mikubwa.  
         Wanawake halmashauri ya Arusha wameungana na wanawake wote duniani kuadhimisha siku muhimu ya Wanawake duniani maadhimisho yaliyoambatana na maonesho ya bidhaa za  wajasiriamali wanawake, upimaji bure  wa afya ikiwemo kansa ya kizazi na kutoa vyeti kwa wadau wa maendeleo ya mwanamke ndani ya halmashauri hiyo, shuguli iliyosimamiwa na Idara ya maendeleo ya Jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.