Wananchi wanaendelea kujitokeza kwa wingi katika Kampeni ya utoaji msaada wa kisheria inafanyika kwenye viwanja vya KKKT Ilkiding'a, huku wanawake wakimiminika kwa wingi, kupata msaada wa kishria bure.
Kina mama hao wameweka wazi kuwa wameridhishwa na huduma hiyo ya kisheria bure, iliyowawezesha kupata elimu ya mambo mengi, ikiwemo haki za watoto, wajibu wa wazazi kwa watoto, umiliki wa ardhi kwa wanawake pamoja na kufahamu umuhimu wa utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala.
Nai Paulo, amebainisha kuwa, kupitia elimu tuliyopata, itapunguza hali ya Unyanyasaji na ukatili dhisi ya wanawake na watoto, kwa kuwa wengi wetu walikuwa gizani.
Mwenyekiti wa Jumuia yawazazi CCM kata ya Ilkiding'a Paulo Ngalabali, amesema kuwa mara nyingi jumuia hiyo, bado watoto wanafanyiwa ukatili ndani ya familia zetu, jumuia imekuwa ikishirikiana na wadau kutoa elimu na mapambano dhidiya ukatili.
"Katika Kampeni hii, tumeshuhudia Waziri mwenye dhamana ya sheria, na watalamu wakisistiza sheria za kuwabana watu wanaofanya matukio ya ukatili dhidi ya watoto na adhabu zake, hivyo tuungane kupambana na ukatili huo". Ameshauri Ngalabali.
Afisa Ustawi wa Jamii, Josina Mlaki, akitoa maelezo ya kazi zinazofanya na kitengo hicho kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Mh. Dkt. Damas Ndumbaro, alipotembelea banda la halmashauri ya Arusha, wakati wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria, kwenye viwanja vya kanisa la KKT lkiding'a.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.