• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANUFAIKA WA MPANGO WA TASAF WA KUNUSURU KAYA MASKINI, WAKIRI KUANZA KUIMARIKA KIUCHUMI

Posted on: November 14th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.


Kaya  zinazonufaika na Mpango wa Kunusuru kaya Maskini kijiji cha Oldonyowas, halmashauri ya Arusha,  mradi unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii -  TASAF awamu ya III, wamekiri kaya hizo kuanza kuondokana na umasikini uliokithiri kwa kujimudu kimaisha kupitia biashara ndogondogo wanazozifanya, zinasaidia kuongeza pato la kaya.

Wakizungumza kwa niaba ya kaya hizo zinazonufaika na mradi huo wa kunusu kaya maskini ,mbele ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za mitaa, wanakaya hao licha ya kuishukuru na kuipongeza serikali, wameweka wazi kuwa kupitia miradi inayofanyw a na TASAF kijijini hapo, zile kaya ambazo zilikuwa maskini sana, zimeanza kubadilika na kuanza kuwa na mpango wa endelevu wa  kujiongezea kipato, tofauti na hapo awali, kaya hizo ziliishi maisha ya kubahatisha.

Lucy Wiliam, mlengwa wa kaya maskini amesema kuwa, mradi wa kupokea pesa za ruzuku pamoja na kupatiwa elimu ya ujasiriamali kupitia vikundi vya wekeza vya kinamama wanufaika wa mradi, wameweza kuweka pesa na kukopeshana, pesa ambazo zimewapa mitaji ya kufanya biashara mbalimbali ikiwemo za mazao ya mboga mboga, ufugaji wa kuku, mbuzi na kondoo, jambo ambalo limeinua kipato cha kaya nyingi na kuzifanya kaya hizo kumudu kupata mahitaji muhimu ya familia

"Wananchi wa Oldonyosambu kwa sasa hawana tofauti na wale wa Dar es salama, watoto wetu wanapata mahitaji yote kama watoto wa mjini, kwa sasa tunauwezo wa kuendesha biashara ndogo ndogo ambazo zinatuwezesha kumudu kukidhi mahitaji ya familia kama chakula cha watoto, tunanunua mahitaji ya shule ya watoto,  tunalipa ada za watoto, yaani TASAF imefanya na sisi watoto wetu kusoma vizuri kama watoto wengine" amesema Lucy.

Hata hivyo wajumbe hao, wamewapongeza wana kaya hao, kwa kuwasistiza kuwa serikali inapata ari ya kuendelea kusaidia jamii, pale ambapo jamii inapokea miradi na kuitekeleza kwa ustadi kama ilivyo kwa wanachi wa Oldonyowas,  wanachi ambao wanafikisha serikali kwenye kusudio lake na kuwasisitiza kuendelea kuunga mkono juhudi hizo za serikali kwa kufanya kazi kwa bidii ili kuondoa umaskini uliokithiri nchini.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya kudumu ya Bunge Utawala na Serikali za Mitaa, Mhe. Abdala Kalembo, amesema kuwa, lengo la miradi ya TASAF ni kuondoa umaskini uliokithiri kuanzia ngazi ya kaya, na kuwapongeza wana kaya hao kwa kutekeleza kwa vitendo adhma hiyo ya serikali na kuwataka kuendelea kushirikiana na serikali kupambana na umaskini uliokithiri katika kaya zao.

"Inaridhisha sana pale unapokuta wananchi wameimiliki miradi inayotekelezwa na serikali kama ilivyo kwa wananchi hawa wa Oldonyowas, kwa kufanya hivi serikali itafikia malengo yake ya kuondoa umaskini kwenye jamii na taifa kwa ujumla" amesisitiza Mheshimiwa Bulembo.

Tangu mwaka 2014, TASAF awamu ya III na mpango wa kunusuru kaya masikini, imetekeleza katika vijiji 45 vya halmashauri ya Arusha na kuzifikia ya  jumla ya kaya 9,107 kwa wamu ya kwanza na kaya 8,112, kwa awamu ya pili, huku kaya hizo zikipokea kiasi cha shilingi bilioni 9.5 kwa mizunguko 28  na jumla ya miradi 46 yenye thamani ya shilingi bilioni 2.1 ilitekelezwa katika sekta ya elimu, afya,  miundombinu ya barabara, uwezeshaji wananchi kiuchumi kupitia vikundi vya kilimo, ufugaji na utunzaji wa mazingira.

ARUSHA DC

KaziInaendelea✍✍

PICHA ZA MATUKIO YA WAJUMBE WA KAMATI YA BUNGE IKIKAGUA MRADI WA KIKUNDI CHA KINAMA

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.