• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WANUFAIKA WA TASAF WAELEKEA  KUFIKIA MALENGO YA MPANGO YA KUONDOA UMASIKINI

Posted on: August 1st, 2022

Na Elinipa Lupembe

Wananchi walio kwenye Mpango wa Kunusu Kaya Masikini kipindi cha pili awamu ya tatu, mradi unaotekelezwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Halmashauri ya Arusha, wamekiri kuanza kuondokana na wimbi la umasikini uliokithiri, uliokuwa ukizikabili kaya zao na kuwa na mwelekeo wa kufikia malengo ya mpango huo.

Wanufaika hao wamekiri fedha hizo, kuwezesha kuondokana na wimbi la umasikini lililokuwa likizikabili kaya hizo, kwa kuanza kukuza kipato cha kaya na kuwezesha kaya kukua kiuchumi na kijamii huku watoto wakipata huduma za afya na elimu  kwa amani na furaha, tofauti na  hapo awali.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti wakati wakupokea ruzuku ya dirisha la 6, wanufaika wa kijiji cha Oloigueruno kata ya Ilkiding'a, wamekiri  fedha hizo za ruzuku kuwezesha kukuza kipato cha kaya kwa kuanzisha miradi na biashara ndogo ndogo.

Helena Lukumai (37), anayejishughulisha na bishara ya uuzaji wa viatu, amesema kuwa, pesa ya TASAF ndio imemuwezesha kupata mtaji wa kuuza viatu na tangu alipoanza kupokea pesa hizo alizikusanya mpaka kufikia shilingi elfu 80 na kupata mtaji wa kuanzisha biashara ya kuuza viatu.

Ameweka wazi kuwa awali hali ya maisha ya kaya yake haikuwa nzuri, hata kupata chakula cha familia ilikuwa ni changamoto, lakini kwa sasa ana uhakika wa famila yake kupata milo mitatu pamoja na kujikimu na mahitaji mengine ya nyumbani.

Naye Judith Paulo amebainisha kuwa, alianzisha mradi wa genge la kuuza mbogamboga, genge ambalo linafanya vizuri na  kwa sasa kaya yake ina uhakika wa maisha, watoto wanapata chakula na mahitaji mengine kupitia genge hilo.
Neema Saitabau kijiji cha Lemanda, anyejishughulisha na biashara ya kuuza viazi soko la Oldonyosmabu, amesema kuwa, alikusnaya pesa za alizopokea TASAF na kupata elfu sitini na kuanza biashara ya kuza viazi kwenye magulio ya Oldonyosambu na Ngaramtoni.

"Nilianza na gunia moja kwa sasa nina mtaji wa magunia matatu, ninauza kwenye masoko ya Oldonyosambu na Ngaramtoni na ninategeme mtaji ukiongezeka kwenda kwenye masoko mengine zaidi". Amesisitiza Neema

Hata hivyo wanufaika hao wameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na mama Samia Suluhu, kwa kutoa elimu bila malipo mpaka kidato cha sita, jambo ambalo wamekiri kusaidia watoto wa kaya za walengwa wa TASAF, kuwa na uhakika wa masomo mpaka kidato cha sita kama ilivyo kwa watoto wengine.

"Zamani ilitulaizimu kutumia pesa hii ya TASAF kulipia watoto ada na michango mingine shuleni, baada ya serikali kuviondoa vyote, tumepata ahueni sana, pesa hizi zinatumika kufanya shughuli nyingine za kutuingizia kipato, kiukweli serikali imeturahisishia maisha kwa kiasi kikubwa mno".Amefafanua Anna Pendaeli

Naye Mratibu wa TASAF halmashauri ya Arusha, Grace Makema, amesema kuwa, kwa mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya shilingi bilioni 2. 8 zimetumika kulipa walengwa hao kwa madirisha 6 huku jumla ya kaya 13,920 kutoka vijiji vyote 88 vya halmashauri hiyo zikinufaika na kuongeza kuwa, malipo yanayofanyika sasa ni dirisha la 6 na jumla ya shilingi milioni 568.8 zimegawiwa kwa kaya hizo.

Ikumbukwe kuwa lengo la Mpango wa kunusuru kaya Masikini kipindi cha pili cha awamu ya tatu mwaka 2020 mpaka 2023 ni kutoa fursa za  kuongeza fursa za kujiongezea kipato na kuboresha huduma za kiuchumi na kijamii kwa kaya za walengwa pamoja na kulinda maslahi ya watoto kiafya na kielimu.


*SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI*

*JIANDAE KUHESABIWA 23 AUGUSTI 2022*.











Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.