• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WATAHINIWA 5,402 KUFANYA MTIHANI WA TAIFA WA KIDATO CHA NNE 2021, ARUSHA DC

Posted on: November 14th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Jumla ya wanafunzi 5,402, wanatarijia kuanza mitihani wa kidato cha IV kesho.Jumla ya watahiniwa 5,402 halmashauri ya Arusha, wilayani Arumeru, wanatarajia kuanza mitihani yao ya Taifa kesho Jumatatu, mitihani ya kuhitimu kidato cha nne mwaka 2021 kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Baraza la Taifa la Mtihani - NECTA.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi, amesema kuwa, watahiniwa hao, watafanya mitihani hiyo kwenye shule za sekondari 48 za  halmashauri hiyo, na kuwatakia  watahiniwa wote kila la kheri katika mitihani yao na kuwataka kufanya mitihani yao kwa utulivu ili waweze kufaulu, kwa kuwa serikali imeshakamilisha taratibu zote kwa sehemu yake.

Pia amewasihi  wasimamizi wote wa mitihani hiyo, kuepuka vitendo vya udanganyifu vitakavyosababisha uvunjifu wa sheria za mitihani ya Taifa, badala yake kuzingatia na kufuata kanuni, taratibu, Sheria na miongozo yote ya mitihani ya Taifa ikiwa ni pamoja na kuzingatia taratibu za  watahiniwa wenye mahitaji maalum.

"Wasimamizi wote wamepewa semina elekezi, mafunzo yaliyowapa uwezo wa kuelewa taratibu zote za mitihani ya Taifa, wanafahamu 'do's na don't' katika usimamizi wa mitihani, serikali imewaamini na kuwapa dhamana hiyo kubwa kwa maslahi ya taifa letu, hivyo kila msimamizi akatekeleze wajibu wake kwa mujibu wa sheria". Amesitiza Mkurugenzi Msumi 

Aidha mkurugenzi huyo, amethibitisha kuwa, maandalizi yamekamilika, na wanategemea kuanza mitihani hiyo kesho, kufuatia ratiba iliyotolewa na Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) na kuthibitisha kuwa watahiniwa wameandaliwa vizuri Kisaikolojia na wanategemea mitihani hiyo itafanyika kwa amani na utulivu. 

Hata hivyo, Kaimu Afisa Elimu Sekondari, halmashauri ya Arusha, mwalimu Safi Mturi, amefafanua kuwa, watahiniwa watakaofanya mitihani hiyo ni pamoja na watahiniwa wa shule (School Canditates), watahiniwa wakujitegemea (Private Candidates) pamoja na watahiniwa wa Maarifa (QT).

Kaimu Afisa Elimu huyo, amefafaanua kuwa, idadi hiyo ya watahiniwa  5, 402, imejumuisha wa tahiniwa wa shule 4,988, ikiwa wavulana 2,061 wasichana 2,887, watahiniwa  398 ni wa kujitegemea huku watahiniwa 56 ni wale wa Maarifa - (QT).

Kaimu Afisa Elimu Safi, amethibitisha kukamilika kwa maandalizi yote kwa mujibu wa taratibu za mitihani ya Taifa, huku halmashauri ikiwa na mategemeo ya watahiniwa hao kupata matokeo mazuri, kutokana na maandalizi yaliyofanywa na walimu shuleni, sambamba na mkakati wa kutokomeza alama sifuri kwa watahiniwa wote wa kidato cha nne, 202.

Naye Mkuu wa shule ya sekondari Ilkiding'a mwalimu Supeet Sailevu, amethibitisha kukamilika kwa maandalizi yote katika shule yake kwa kuzingatia miongozo na taratibu zote, na kuongeza kuwa wanafunzi wa shule hiyo, wameandaliwa vizuri kisaikolojia, lakini pia wamefanya majaribio na mitihani mingi ambayo imewafanya kujiamini katika mitihani.

"Tunategemea wanafunzi wetu kupata matokeo mazuri, kwa kuwa kila mwalimu wa somo, amemaliza mada zote, na kuwandaa vema kwa mtihani huu wa Taifa, wanafunzi wamefanya mitihani mingi sana, kiasi cha kuwafanya wanafuzni wetu hawaogopi mitihani, iliyobaki tuwaombee tuu" amesema Mkuu huyo wa shule.

Halmashauri ya Arusha inawatakia watahiniwa wote, kila la Kheri katika mitihani yao, kufanya mitihani kwa amani na utulivu ili kupata matokeo mazuri.





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.