Mafunzo kwa Watalamu, viongozi na Vijana wa Kata ya Bwawani, wataakofanya kazi ya kupanga na kukusanya taarifa za Anwani za Makazi halmashauri ya Arusha, yamefanyika kwenye shule ya sekondari Olokii kata ya Bwawani.
Mafunzi hayo yenye lengo la kiwajengea uwezo watalamu, viongozi na vijana wa ngazi ya kata, vijiji na vitongoji wa kutekeleza zoezi la kukusanya taarifa na kupanga Anwani za Makazi katika kata ya Bwawani.
Mafunzo hayo yaliambatana na zoezi la vitendo la kuandika namba za nyumba Zoezi hilo linategemea kuanza rasmi katika kata zote 27, vivijiji 67 na vitongoji 256 vya halmashauri ya Arusha, wananchi wote wanatakiwa kutoa ushirikiano ili kukamilisha zoezi hilo la Kitaifa.
Ewe Mwananchi hakikisha unatoa ushirikiano kwa watalamu watakaopita kwenye Makazi yenu kukusanya taarifa.
ARUSHA DC
KaziInaendeleaa✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.