• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WaterAid NA HEDHI SALAMA SHULE ZA PEMBEZONI ARUSHA DC

Posted on: September 24th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Shirika lisilio la kiserikali la WaterAid Tanzania limetoa msaada wa taulo za kike 660, kwa wasichana wanaosoma shule za sekondari za pembezoni, halmashauri ya Arusha, lengo likiwa ni kuwapa wasichana uhakika wa hedhi salama isiyokuwa  na vipingamizi na kuwapa uhakika wa kuhudhuria masomo kipindi chote cha masomo hata wakiwa kwenye hedhi.

Akizungumza wakati akigawa taulo hizo kwa maafisa Maendeleo ya Jamii wa kata, Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, Mhe. Ojung'u Salekwa, amelishukuru shirika kwa msaada huo muhimunkwa mtoto wa kike na kusisitiza kuwa kumuelimisha mtoto wa kike ni kuelimisha jamii, hivyo kuondoa changamoto kwa mtoto wa kike ni kuiondolea jamii changamoto.

Mkurugenzi  Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi licha ya kuwashukuru wadau wa WatetAid, kwa kutambua thamani ya mtoto wa kike kwa kumuwezesha kujiamini wakati wa hedhi.

"Tunafahamu changamoto ni kubwa kwa watoto wa kike, hasa maeneo ya vijijini, wengi hukosa vifaa vya kujihifadhi na kulazimika kutokuhudhuria masomo, kwa msaada huu, WaterAid wamesaidia kupunguza tatizo hilo katika halmashauri yetu". Amefafanua Msumi.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Mkuu, halmashauri ya Arusha, Angela Mvaa, amesema kuwa ugawaji wa taulo hizo utaenda sambamba na utoaji wa elimu ya kujitambua kwa wasichana ili kukabiliana na changamoto za kijamii, ikiwemo makuzi na mabadiliko ya mwili pamoja na athari za mahusiano ya kimapenzi katika umri mdogo.

"Tumeshuhudia vijana wanauana na wengine kujiua kwa ajili ya mahusino, hivyo tumeamua kuanza kuwapa elimu ya mahusiano na athari zake na namna ya kuishi katika mahusiano kwa kukabiliana na changamoto zake bila kuathiri uhai wa mwingine" . Amesisitiza Angela

Hata hivyo Afisa Elimu kata ya Bwawani, Mwl. Edward Mbesere, amethibitisha uwepo wa tatizo la wasichana kukosa taulo za kujihifadhi wakati wa hedhi na kusababisha kushindwa kuhudhuria masomo kila mwezi, kutokana na uwezo mdogo wa familia na kulifanya tukio hilo ni la siri miongoni mwa wanajamii.

"Mara nyingi msicha akisha vunja ungo, anaomba ruhusa ya kuumwa kila mwezi, ukifuatilia utagundua msichana hakufika shule kwa sababu yuko kwenye siku zake, na sio kwamba anaumwa ni kukosa vifaa vya kujistiri na kuamua kukaa nyumbani." Ameweka wazi Mwl. Mbesere  

Awali shirika la WaterAid Tanzania limetoa jumla ya taulo za kike 660, ambazo zimegawiwa kwa shule  za sekondari za Olokii, Musa, Sambasha, Oljoro, Losinoni, Losikito, Mukulat na Einotj zote zikiwa kwenye kata za mbali na miji.


ARUSHA DC 

TUPO KAZINI✍✍


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA MAKABIDHIANO YA TAULO ZA KIKE


Mwenyekiti halmashauri ya Arusha, Mhe. Ojung'u  Salekwa, akimkabidhi taulo za kike, Afisa Maendeleo ya Jamii kata ya Lemanyata   Nsia,

 Marasa,  kwa ajili ya kuzigawa kwa shuke ya sekondari Mukulat.







 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.