Na Elinipa Lupembe
Jumla ya watoto 7 wamezaliwa wakati wa mkesha wa mwaka mpya katika vituo vya afya halmashauri ya Arusha.
Mratibu wa uzazi halmashauri hiyo Sista Bujiku Butolwa amesema kuwa wakati wa mkesha wa mwaka mpya wa 2023 jumla ya wajawazito 16 walipokelewa huku 10 kati yao wakiwa na hali ya uchungu na baadaywa kina mama 7 kati yao walijifungua na hali za watoto na kina mama wote zinaendelea vizuri.
"Kati ya kina mama hao, kina mama wawili walijifungua kawaida na wawili walijifungua kwa njia ya upasuaji lakini afya za kina mama na watoto wote waliozaliwa wanaendelea vizuri". Amesema Sista Bujiku.
Aidha Sista Bujiku ameendelea kuwasisitiza wajawazito kujigungulia kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na kuwataka kina mama waliojifungua kuwanyonyosha watoto hao kwa siku 1000 za mwanzo.
Hata hivyo ameitaka jamii kuendelea kuwahudumia kina mama waliojifungua kwa kuhakikisha wanapata lishe bora kipindi chote cha uzazi ili kulinda afya za watoto waliozaliwa.
Uongozi wa Halmashauri ya Arusha, inatoa hongera kwa kina mama wote waliojaliwa kupata watoto na kuwatakia afya njema.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.