• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WATOTO ARUSHA DC WAMEWATAKA WAZAZI KUHESHIMU HAKI ZAO

Posted on: June 16th, 2021

Na Elinipa Lupembe.

Watoto halmashauri ya Arusha, wamewataka  wazazi kutambua na kuheshimu haki zao, kwa kuacha kuwafanyia vitendo vya ukatili, vitendo ambavyo vinakatisha ndoto za maisha ya watoto wengi, pamoja na kuathiri maisha yao kisaikolijia.

Watoto hao wamewasilisha vilio vyao, kupitia jumbe mbalimbali walizoziwasilisha kupitia sanaa ya ngoma, nyimbo, mashairi, ngonjera na mashairi, wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika, yaliyofanyika kewenye viwanja vya shule ya msingi Musa iliyoko kata ya Musa.Namnyaki Mollel, mwanafunzi wa darasa la tano, shule ya msingi Nengung'u, ameweka wazi kuwa watoto wengi hufanyiwa ukatili na watu wao wa karibu, ambao huishi ndani ya famili na jamii zetu, tunaomba wazazi kuachana na mila potofu inayoruhusu mtoto kuozeshwa katika umri mdogo, tabia ambayo imejengeka kwenye jamii yetu. 

"Tunaomba wazazi wetu, kuachana na mila na desturi potofu, zinazochangia vunjifu wa haki za watoto, tunaomba wazazi wetu  msituozeshe katika umri mdogo, lakini pia wazazin hakikisheni kila mtoto anapata haki zake za msingi zinazomuwezesha mtoto kupata makuzi bora" amesisistiza Namnyaki.

Aidha watoto hao, wameiomba serikali kulinda haki zao, kwa kusimamia kesi za watoto, waliofanyiwa ukatili, kesi ambazo mara nyingi humalizika bila kupata suluhisho na kwanyima haki watoto wengi.Naye mgeni rasmi, akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi Mtendaji, Mwanasheria wa halmashauri ya Arusha, Monica Mwailolo amewakumbusha wazazi na jamii, kufanyia kazi malalamiko yaliyowasilishwa na watoto, na kuwasihi wazazi kuachana na mila na desturi zinazowafanyia ukatili watoto kwa kuhakikisha kila mzazi anatekeleza jukumu lake katika malezi.

"Wazazi mna jukumu kubwa la kutekeleza haki za watoto, na kuwalinda watoto, kama wazazi mataacha kuwaozesha watoto katika umri mdogo, kuwakeketa na kuwatelekeza, tutakuwa na jamii yenye kutekeleza, haki za watoto kufuatia agenda 2040 kama ilivyo kauli mbiu ya kuifanya Afrika inayotekeleza Haki za watoto 2040" amesistiza mgani rasmi huyo.

Aidha umeainishwa ukatili unaofanya dhidi ya watoto ni pamoja na ndoa za utotoni, kukeketwa, kubakwa na kulawitiwa, kufanyishwa kazi, pamoja na kutelekezwa na kuwasisitiza jamii, kusimamia na kupambana dhidi ya ukatili huo, unaofanywa na jamii kwa watoto. 

Maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika huadhimishwa kila tarehe 16.06 ya mwaka, halmashauri ya Arusha imeungana na mataifa 51 duniani kuadhimisha siku hiyo maalum, kwa kushirikaiana na wadau wa mashirika ya ACE AFRICA,  CWCD, COMPASSION, DORCAS AID, KIZAZI KIPYA, ELCT - KKP, maadhimisho yaliyobeba  Kauli Mbiu "Tutekeleze Ajenda 2040: Kwa Afrika inayolinda Haki za Mtoto.

PICHA ZA MATUKIO.







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.