• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Watoto wameiomba Serikali kutatua changamoto zinazowakabili ili kuwaandaa kuelekea uchumi wa viwanda

Posted on: June 12th, 2018

Kufuatia Kauli mbiu ya siku ya mtoto wa Afrika mwaka 2018,  inayosema 'KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA:TUSIWAACHE WATOTO NYUMA', watoto wameiomba serikali kutatua changamoto nyingi zinazowakabili ambazo zinakwamisha maendeleo na ustawi wa watoto, kuelekea uchumi wa viwanda.

Rai hiyo ya watoto, imetolewa  na Mwenyekiti wa Baraza la Watoto Tanzania, Joel Festo wakati akiwasilisha maazimio ya watoto, kwenye Kongamano la watoto mkoa wa Arusha, lililofanyika kwenye ukumbi wa Lake Nyasa ndani ya kituo cha kimataifa cha mikutano AICC.

Mwenyekiti Joel amesema kuwa, changamoto zinazowakabili watoto kwa sasa, zinatakiwa kudhibitiwa na kutafutiwa ufumbuzi,  endapo hazitatafutiwa ufumbuzi endelevu, zinaweza  kuleta madhara makubwa kwa maisha ya watoto baadae na watoto kushindwa kufikia malengo ya kutekeleza uchumi wa viwanda.

Mwenyekiti huyo amezitaja baadhi ya changamoto hizo ambazo ndio maazimio ya Baraza la watoto kuwa, ni pamoja ukosefu wa miundombinu ya shule isiyorafiki, ambayo inakwamisha tendo la kujifunza na kusababisha watoto wengi, kushindwa kufanya vizuri katika masomo, huku hali hiyo ikitishia watoto hao kutokuendana na matarajio ya serikali ya kuwa na wasomi wa kimkakati, kuelekea kwenye uchumi wa viwanda.

Joel ameendelea kueleza kuwa, vitendo vya ukatili dhidi ya watoto vinavyofanywa na jamii, ajira za watoto hasa watoto wanaoishi maeneo ya migodini na kwenye mashamba makubwa, kukeketwa, mimba na ndoa za utotoni, haviwezi kuwafanya watoto kufikia uchumi wa viwanda unaoandaliwa na serikali kwa sasa.

Ameongeza kuwa, watoto bado wanachangamoto ya ushirikishwaji hafifu wa kutoa maamuzi kuanzia ngazi ya familia, Huduma za afya kwa watoto hasa maeneo ya vjjini, adhabu kali zenye madhara kwa watoto,pamoja na mahakama zisizo rafiki za kuuendeshea mashauri  na kesi za watoto.

" Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya, baba yetu, watoto wanakuomba, kutatua changamoto hizo ili kuwaandaa watoto hawa, kuelekea kwenye uchumi wa viwanda, kwani watoto  wa Tanzania, wanayo matarajio makubwa ya kutekeleza uchumi huo pindi watakapokuwa watu wazima" amesema Mwenyekiti Joel.

Hata hivyo Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, mheshimiwa Faustine Ndugulile amesema kuwa serikali inafahamu changamoto za watoto na imeweka mikakati thabiti ya kutatua changamoto hizo kisekta.

Mpaka sasa serikali pamoja na kutoa elimu bila malipo lakini pia, inaendelea kuboresha miundombinu ya shule na kuwa na mazingira rafiki ya kujifunzia ili kupata wasomi wa kuendeleza taifa hili.

Ameongeza kuwa serikali, imeandaa sera  na sheria ya mtoto huku ikianzisha mahakama za watoto zenye mazingira wezeshi ya kufanyia mashauri ya watoto, mahakama zitakazoshughulikia mashauri ya matukio ya ukatili dhidi ya watoto,pamoja na kuwa na jela maalum ya watoto ambayo watoto wataendelea kupata haki zote za msingi wakiwa huko.

"Serikali inatambua changamoto za kufanya mashauri ya watoto kwenye mahakama zilizopo, kwa sasa kutakuwa na mahakama za watoto zenye mazingira huru kwa mtoto, zaidi kutakuwa na jela za watoto".  Amesema Naibu Waziri

Naibu Waziri huyo, amefafanua kuwa licha ya serikali kuweka mikakati hiyo, ameitaka jamii  kushirikiana na serikali, kuwaandaa watoto kuelekea uchumi wa viwanda kuanzia ngazi ya familia, kwa kuwapa haki zote za msingi huku jamii ikiwa na kazi kubwa ya kuwalinda watoto.

Aidha amewataka watoto wenyewe kujilinda na kutambua haki zao na kutoa taarifa pale wanapofanyiwa vitendo vya ukatili kupitia namba maalumu ya 116 na kupitia kwa viongozi wa maeneo wanayoishi na kutumia madawati ya malakamiko yaliyoanzishwa shule.

"Watoto serikali yenu inawapenda na kuwajali, msiogope na wala msikubali kunyamazishwa na mtu yoyote pale unapofanyiwa aina yoyote, serikali ipo kwa ajili yako na itakulinda" amesisitiza Naibu Waziri

Awali katika kongamano hilo, watoto wamepata fursa ya kujadili mambo mbalimbali yanayowahusu huku wakijengewa uwezo wa namna ya kukabiliana na changamoto zinazowakabili hasa ukatili dhidi yao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.