• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAUGUZI ARUSHA DC WAKUMBUSHWA MSINGI NA MAADILI YA UUGUZI..

Posted on: July 13th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Wauguzi halmasahuri ya Arusha, wametakiwa, kutoa huduma rafiki kwa wagonjwa kwa kufanya hivyo kutawafanya wagonjwa kujisikia wanapata ahueni kabla ya hata ya kupatiwa matibabu na dawa.

Rai hiyo imetolwa na Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, wakati akifungua semina ya Wauguzi wa halmasahuri hiyo, ya kukumbushana namna ya utekelezaji wa majukumu yao na misingi na maadili ya taaluma ya uuguzi.

Mkurugenzi Msumi, amefafanua kuwa taaluma ya uuguzi ni wito ambao unamlazimu muuguzi kujitoa kabla ya kuweka maslahi mbele kwa kutumia lugha nzuri kwa mteja wake, ili kumfanya mgonjwa ajisikie yuko kwenye mikono sahihi tayari kwa kupata uponyaji.

"Mtu anapokuwa mgonjwa kwanza hayuko sawa kiakili, kimwili na kisaikolojia, huduma ya kwanza anayotakiwa kupewa ni faraja na upendo, kwa kufanya hivi mgonjwa anaanza kupona kabla hata ya kupata matibabu yenyewe, mkishindwa kufanya hivyo, malalamiko yote ya wagonjwa yanakuja kwa serikali, fanyeni kazi kwa uadilifu ili kufikia malengo ya serikali" Amesisitiza Msumi

Aidha amewakumbusha wauguzi hao kuwa Serikali imewaamini na kuwapa jukumu la kuwahudumia watanzania ambao ni wagonjwa, ni vema kila mtu akatimiza majukumu yake huku akiweka mbele uzalendo, utayari, utii, uwazi na uwajibikaji, ili kufikia lengo la serikali la kutoa huduma bora kwa jamii.

Hata hivyo wauguzi hao, wamefurahishwa na semina hiyo, ambayo wamekiri imewapa fursa ya kubadilisha uzoefu wa namna ya kutatua changamoto zinazowakabili wauguzi katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku na kuipongeza serikali ya mama Samia kwa kuendelea kuboresha miundominu ya Afya pamoja na upatikanaji wa dawa na vifaa tiba, jambo ambalo linawapa moyo na ari ya kufanya kazi na kuwahudumia wagonjwa kwa bidii.

Nmnyaki Lazaro muuguzi kituo cha afya Nduruma amesema kuwa, wao kama wauguzi, wana jukumu kubwa la kuwahudumia wagonjwa kwa kuzingatia uwajibikaji wenye tija na kutoa huduma bora na rafiki kwa wagonjwa bila kujali  changamoto zinazowakabili katika maeneo yao ya kazi.
   
Modeta Patrick, muuguzi zahanati ya Ngorbon amethibitisha kuwa kupitia mafunzo hayo, wamejipanga kutoa huduma bora inayozingatia misingi na maadili ya taaluma ya uuguzi hususani katika eneo la huduma bora kwa mteja.

Naye Muuguzi Mkuu, halmashari ya Arusha Neomi Temu, amesema kuwa, lengo la semina hiyo ni,   kuwakumbusha wauguzi hao namna bora ya utekelezaji wa majukumu yao hususani katika kipengele cha huduma bora kwa mteja, huduma ambayo ikitolewa kwa ufasaha, inaleta faraja kubwa kwa wagonjwa na kuendelea kuiamini taaluma ya uuguzi.

Inafahamika kuwa asilimia 80 ya wahudumu katika sekta ya afya ni Wauguzi, hivyo wakiwekewa mazingira rafiki ya kutoa huduma kwa wagonjwa, na wao kujituma na kufuata misingi na maadili ya kazi yao, iitapunguza malalamiko na kuongeza ufanisi katika fani ya utabibu nchini.

ARUSHA DC
KaziInaendelea
JIANDAE KUHESABIWA


PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA MAFUNZO YA WAUGUZI


Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, akifungua semina ya Wauguzi iliyofanyika katika ukumbi wa halmasahuri ya Arusha






Mganga mkuu wa halmashauri ya Arusha, Dkt. Petro Mboya akiongea na wauguzi wa halmashauri ya Arusha 


Wauguzi wakiwa katika semina ya Wauguzi  ya kukumbushana namna ya utekelezaji wa majukumu yao na misingi





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.