• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Wauguzi Arusha DC watakiwa kuwahudumia wagonjwa wakionesha tabasamu na bashasha

Posted on: July 24th, 2019

Wauguzi na watabibu halmashauri ya Arusha wilaya ya Arumeru, wameatakiwa kutoa huduma za afya kwa wagonjwa, kwa kuzingatia weledi, maadili na miiko ya taaluma zao, ili kuendana na kasi ya Serikali ya awamu ya tano ya kuwahudumia wananchi wanyonge.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Jerry Muro wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kampeni ya kitaifa ya 'JIONGEZE TUWAVUSHE SALAMA' katika halmashauri ya Arusha, kampeni yenye lengo la kutokomeza vifo vya mama na mtoto, vitokanavyo na uzazi.

Mkuu huyo wa wilaya, amewataka wahudumu wote wa afya katika halmashauri hiyo,  kuwahudumia wagonjwa kwa kuzingatia maadilo huku, wakiwa na tabasamu na bashasha la moyo, kwani kwa kufanya hivyo kunawapa wagonjwa matumaini ya kupona kabla ya kupata huduma nyingine za kitabibu zinazohitaji utalamu zaidi.

"Mgonjwa anapofika hospitali, jambo la kwanza anahitaji faraja, faraja inayotokana na tabasamu lako, pindi unapompokea, tabasamu inampa mgonjwa matumaini ya kupona haraka, kabla ya kupatiwa huduma nyingine za vipimo na dawa, wauguzi mtusaidie kufanya jambo hilo, halihitaji maarifa makubwa ni moyo wa kujitolea " amesisitiza Mkuu huyo wa Wilaya.

Aidha amewaonya wauguzi, kuacha tabia ya kutumia muda mwingi kwenye simu za mkononi kwa kuchati, wakati wawapo kazini,jambo linalowakwaza wagonjwa, badala yake kutumia muda huo kuwasikiliza na kuwahudumia wagonjwa na kuongeza kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi kuboresha huduma za afya, hivyo jukumu lao kubwa ni kuwahudumia wagonjwa wa aina zote.

"Natoa onyo kwa wahudumu wa afya kuacha tabia ya kuchart muda wa kazi, tunawafuatilia na hatutasita kuwachukulia hatua za kinidhamu, watumishi wanaokiuka taratibu za kazi, kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao" amesema Muro.

Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Dkt. Wilson Mahera, amethibitisha hatua kubwa iliyofikiwa katika halmashauri yake katika sekta ya afya, kwa kuboresha miundombinu ya afya na uwepo wa dawa na vifaa tiba katika halmashauri hiyo, na kuwataka wahudumu wa afya kuwajibika kutoa huduma bora za afya katika maeneo yao ya kazi.

Naye Mganga Mkuu, Halmashauri ya Arusha, Dkt. Peter Mboye, ameweka wazi kuwa, chanzo cha vifo vya uzazi ni kutokwa na damu nyingi wakati wa kujifungua, kifafa cha mimba na wajawazito kuchelewa kufika hospitali wakati wa uchungu, na kuongeza kuwa, ili kukabiliana na uzazi pingamizi, halmashauri imejipanga kukabiliana na changamoto hizo, kwa kuelimisha jamii kuwawahisha wajawazito kufika vituo vya afya waonapo dalili za uchungu, pamoja na kukusanya damu salama kutoka kwa kuwahamasisha wananchi kujitolea damu.

Muuguzi Mkuu, halmashauri hiyo, Sista Agusta Komba, amesema kuwa, licha ya vifo vya mama na mtoto kupungua, bado mila na desturi za jamii ni changamoto kwa uzazi salama, kutokana na wajawazito kuendelea kujifungulia nyumbani kwa wakunga wa jadi, huku wanaume wakiwa kikwazo cha kutokuhudhuria Kliniki pindi wenza wao wanapokuwa wajawazito.

Awali, Kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama, inasisitiza  mama mjamzito akivuka Salama, mtoto atavuka salama, Familia itavuka salama na nchi itavuka salama.










Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.