Na Elinipa Lupembe
Wawezeshaji 40 ngazi ya wilaya, wamepatiwa mafunzo kwa ajili ya kwenda kufundisha kaya zilizo kwenye Mpango wa Kunusuru Umasikini, mradi unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii ( TASAF IV), kuunda vikundi vya kujiwekea akiba.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo ya siku tano, Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Arusha, Elizabeth Ngobei, amewataka watalamu hao, kutumia maarifa watakayopata kuwezesha jamii kujiunga kwenye vikundi ili kujiinua kijamii na kijamii.
Amewataka watalamu hao kutumia fursa hiyo kuwezesha wanakaya kujiunga kwenye vikundi pamoja na kuhakikisha vikundi hivyo vinatekekeza majumu yao kulingana na mpango taratibu zilizowekwa na TASAF.
"Mnalo jukumu kubwa la kuhakikisha wanakaya hasa kina baba kutambua umuhimu wa kujiunga kwenye vikundi vya huduma ndogo za fedha, na si kuwaachia wa wanawake peke yao, jambo ambalo linaleta mogogoro kwenye kaya, kina baba wanatakiwa kufahamu pesa za TASAF ni la kaya nzima".Amesisitiza Kaimu Mkurugenzi
Hata hivyo Mratibu wa huduma za Vikundi TASAF Makao Makuu, Ester Kivuyo, amesema kuwa lengo mafunzonhayo ni kuzijengea uwezo kaya za walengwa kuwa na utamaduni wa kujiwekea akiba na kutumia akiba hizo katika kukopeshana katika vikundi ili kuendeleza miradi ya kiuchumi ili kujionhezea kipato cha kaya.
Hata hivyo Mratibu wa TASAF, Halmashauri ya Arusha, Grace Makema, amesema kuwa lengo la mafunzo kwa watalamu hao ni kuwajengewa uwezo watalamu watakao kwenda kuzifundisha kaya ngazi ya kijiji.
Amafafanua kiwa mambo muhimu yatakayofanywa na wawezshaji hao ni kuwafundisha wanakaya, uanzishwaji na usajili wa vikundi, uongozi wa vikundi, uandaaji wa katiba, elimu mwendo kwa vikundi, kuweka akiba na kuwekeza pamoja na usimamizi wa mikopo, utunzaji wa kumbukumbu na urejeshaji wa mikopo.
Awali zoezi hili la mafunzo ngazi linategemea kufanyika kwenye halmashauri 13 za mikoa ya Arusha na Njombe huku halmashauri ya Arusha ikiwa miongoni mwake.
"ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"
#kaziinaendelea✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.