Na Elinipa Lupembe.
Wazazi na walezi wametakiwa kuwasimamia watoto wao, katika matumizi ya vifaa vya kielekroniki ili kuwaepusha kujiingiza katika vitendo vya ngono na ukatili mwingine kupitia taarifa zilizopo mitandaoni.
Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, Jijini Dodoma, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yanayoadhimishiwa tarehe 16, Juni kila mwaka.
Waziri Ummy amesema, kuwa katikanyakati hizi, tumeshuhudia watoto wanatumia vifaa ya kielektroniki, ikiwa pamoja na simu na kompyuta kwa lengo la kujifunzia mambo ya masomo, hivyo ni vyema wazazi kuwasimamia watoto wao katika mayumizi ya vifaa hivyo, na kuhakikisha wanazingatia matumizi sahihi ya vifaa hivyo ili kuepusha kuanza kuiga na kufanya vitendo vya kikatili.
Amewasisitiza Wazazi na Walezi kuhakikisha, Usalama wa watoto wakati wote wakiwa nyumbani, katika kipindi hiki pamoja nakuwazuia kwenda kwenye maeneo hatarisgi kwa usalama wao kwa kufanyiwa vitendo vya ukayili, ikiwa ni pamoja na kubakwa, kulawitiwa, kushawishiwa kufanya ngono na hata kupata maambukizi ya Corona.
“Katika eneo la malezi ya watoto wetu bado tuna changamoto kubwa ya matumizi ya mitandao, wazazi na walezi tuhakikishe tunawasimamia watoto wetu wasijiingize katika masuala yasiyofaa katika mitandao hiyo” alisema Waziri huyo.
Aidha Waziri Ummy amaesema kumekuwa na ongezeko la matukio ya vitendo vya ukatili wa kijinsia nchini, kutokana na ukweli kuwa, wananchi wengi wamepata uelewa na kuweza kutoa taarifa katika maeneo maalum yaliyoainishwa na Serikali.
Hata hivyo Waziri Ummy, ameweka wazi takwimu za mikoa ya kipolisi iliyoongoza kuwa na matukio mengi zaidi ya ukatili dhidi ya watoto kwa mwaka 2018 ni Mkoa wa Tanga (1,039), Mbeya (1,001), Mwanza (809) na Arusha (792) na kwa mwaka 2019 ni Mkoa wa Tanga (matukio 1,156), Mkoa wa Kipolisi-Temeke (844), Mbeya (791) na Mwanza (758).
Naye Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maendeleo ya Mtoto Sebastian Kitiku, amewasisitiza wazazi kuwajibika katika malezi kwa kuhakikisha wanawasimamia watoto wao kwa kufuatilia kwa karibu masuala ambayo yanaweza kusababisha ukatili kwa watoto.
“Wazazi tuwaangalie watoto wetu tusiwaache watoto wakajiamulia baadhi ya vitu ambavyo vitawasababisha waingie katika mambo ambayo yatapelekea kufanyiwa vitendo vya kikatili” alisema Kitiku.
Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika kwa mwaka 2020 yenye Kauli mbiu ya “Mifumo Rafiki ya Upatikanaji Haki ya Mtoto: Msingi Imara wa Kulinda Haki Zao”
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.