• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI OLDONYOWAS SEKONDARI WATAKIWA KUCHANGIA CHAKULA CHA MCHANA CHA WATOTO WAO

Posted on: August 28th, 2019

Na Elinipa Lupembe.

Wazazi wenye watoto shule ya sekondari  Oldonyowas, halmashauri ya Arusha, wametakiwa kukaa na kutafakari namna bora, ya kuwapatia watoto wao chakula cha mchana wawapo shuleni.

Rai hiyo imetolewa na Kaimu mkurugenzi,  halmashauri ya Arusha, Anastazia Tutuba, wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa majengo ya shule hiyo na wadau, waliofadhili ujenzi wa majengo shuleni hapo, mara baada ya mkuu wa shule hiyo, kuwasilishwa changamoto ya ukosefu wa chakula cha mchana kwa wanafunzi.

Kaimu mkurugenzi huyo amesema, anasikitishwa sana kusikia wanafunzi, wanafika shuleni saa moja mpaka saa kumi jioni, bila ya kula kitu chochote huku wazazi wakipongezana kwa kuchanga fedha na kujenga shule.

Amesema kuwa shule hiyo ni mpya, ina mandhari nzuri na mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia, endapo watoto hao watashinda njaa, wasitegemee ufaulu kwa wanafunzi hao, badala yake nguvu zao walizowekeza kwenye ujenzi wa shule hiyo, zitakuwa zinapotea bure.

"Mtoto hawezi kufanya vizuri kwenye masomo akiwa na njaa, kwani mtu anaposoma ubongo unapoteza 'carolis' nyingi kuliko mtu anayelima, sasa ili nguvu mlizowekeza shuleni hapa ziweze kuzaa matunda bora kitaaluma, ni lazima muwape watoto hawa chakula cha mchana wawapo shuleni" amesema Kaimu mkurugenzi huyo.

Awali mkuu wa shule hiyo, mwalimu Richard Mugabiso, akisoma risala fupi ya shule hiyo mpya iliyoanza Januari mwaka huu, amethibitisha kuwa, licha ya shule hiyo kujitosheleza kwa miundombinu na walimu, changamoto kubwa ni wanafunzi kutokupata chakula cha mchana wawapo shuleni, jambo linalotokana na wazazi kutokuchangia chakula hicho.

Mkuu huyo wa shule ameonyesha hofu yake, inayoweza kuchangia watoto hao kushindwa kufanya vizuri kitaaluma, kutokana na wanafunzu hao kushinda njaa, kutwa nzima na kuwataka wazazi kuliangalia na kulitafakari suala hilo upya.

Hata hivyo sera ya elimu bila malipo, imefafanua jukumu la wazazi ni kumpatia mtoto mahitaji yake binafisi ikiwemo chakula cha mchana kwa shule za kutwa, madaftari, nauli ya kwenda na kurudi shuleni.

Naye Mwenyekiti wa kijiji cha Oldonyowas, Geofray Ayo amesema kuwa, wazazi wa kijiji cha Oldonyowas, wanajitoa sana kuchangia maendeleo ya shule ikiwemo  chakula cha watoto wao, lakini changamoto kubwa ni wazazi wenzetu wa vijiji vya jirani, wao hawachangii chakula jambo ambalo linasababisha kukosekana kwa chakula.

Hata hivyo, mwenyekiti huyo amasema, wamepanga kukutana na viongozi wa vijiji jirani ambavyo wanafunzi wanatokea, ili kupanga  mkakati wa kuchangia chakula cha wanafunzi.





Kaimu mkurugenzi halmashauribya Arusha, Anastazia Tutuba akizungumza na wananchi wa kijiji cha Oldonyowas, wakati wa makabidhiano ya majengo ya shule ya sekondari Oldonyowas.


Mwenyekiti wa kijiji cha Oldonyowas, mheshimiwa Geofray Ayo, akisoma taarifa ya shule ya sekondari Oldonyowas, wakati wa makabidhiano ya majengo ya shule hiyo.



Wanafunzi wa shule ya sekondari Oldonyowas, wakiwa kwenye hafla ya makabidhiano ya majengo ya shule ya sekondari Oldonyowas.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.