Na Elinipa Lupembe.
Wazazi halmashauri ya Arusha, wamewataka kuhakikisha wanawapa watoto na familia lishe bora, ili kuwakinga na magonjwa na utapiamlo uliokidhiri, kwa kuwa lishe bora ndio msingi wa familia bora na Taifa bora.
Rai hiyo imetolewa na Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndugu Sahili Nyanzabara Geraruma, kwenye mradi wa Kituo cha Kutoa Virutubisho kwa watoto wenye utapiamlo, kituo kinachoendeshwa na Asasi ya Kiraia ya Walk in Love Tanzania, amesisitiza kuwa lishe bora ni muhimu kwa watoto kwa kuwa ndio inayomjenga na kumuwezesha mtoto kukua kimwili, kisaikoloji na kiakili.
"Mtoto anapopata lishe bora kuanzia mdogo itamkinga na maradhi menginikiwemo utapiamlo, lakini zaidi, inamuwezesha kukua vizuri na hatimaye kuwa mjenzi wa taifa letu, watoto ni taifa la kesho ni vema, wazazi tutekeleze jukumu letu la kuwapa lishe bora" amesisistiza Kiongozi huyo wa Mwenge wa Uhuru.
Aidha amewataka wazazi pia kuzikinga familia zao dhidi ya ugonjwa wa malaria, kwa kutumia vyandarua vyenye dawa pamoja na kuwapeleka watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano kliniki, pamoja na kuzingatia maelekezo wanayopewa na watalamu wa afya.
Katika mradi huo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, aligawa chakula lishe na vyandarua kwa kina mama ambao wanahudumiwa na kituo hicho cha Lishe.
Hata hivyo kina mama hao wameishukuru shirika hilo kupitia serikali kwa huduma hiyo wanayoipata, huduma ambayo imesaidia kuokoa maisha ya watoto wao.
Kauli Mbiu ya Mwenge wa Uhuru: Sensa ni Msingi wa Mipango ya Maendeleo, Shiriki Kuhesabiwa, tuyafikie Maendeleo"
Mwenge wa Uhuru Oyeee
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndugu Sahili Nyanzabara akizungumza na wakazi wa Mateves wakati alipotembelea Kituo cha KUutoa Lishe kwa watoto wenye utapiamlo.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndugu Sahili Nyanzabara akiwakabidhi vyandarua kinamama wanaohudumiwa katika Kituo cha KUutoa Lishe kwa watoto wenye utapiamlo, kilichopo kata ya Matevesi.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndugu Sahili Nyanzabara akiwakabidhi Chakula Lishe kinamama wanaohudumiwa katika Kituo cha KUutoa Lishe kwa watoto wenye utapiamlo, kilichopo kata ya Matevesi.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.