Na Elinipa Lupembe
Halmashauri ya Arusha imefanikiwa kuwagawia msaada wa chakula wazee 25 wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani 2023 yaliyofanyika kijiji cha Nduruma kata ya Nduruma.
Akikabidhi chakula hicho Mwenyekiti halmashauri ya Arusha, Mhe.Dkt. Ojung'u Salekwa amesema kubwa halmashauri imetoa chakula hicho kama ishara ya upendo na kuwajali wazee wenye uhitaji.
Amesema kuwa serikali inatambua haliduni za kiuchumi kwa baadhi ya wazee na inaendelea kutatua changamoto hizo kwa kuwaingiza kwenye mpango wa kunusuru kaya masikini, mradi unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF.
Amefafanua kuwa licha ya kuwa kuna malalamiko ya baadhi ya wazee kutokuwepo kwenye mpango, amewataka kuwa wavumilivu kwa kuwa bado serikali inaendelea kufanya uhakiki wa kaya zenye uhitaji ambazo haziko kwenye mapngo wa TASAF kwa awamu na pindi ukikamilika kaya hizo zitaingizwa kwenye mpango huo.
Hata hivyo amewataka watoto kuendelea kuwahudumia wazazi wao bila kuchoka wala kukata tamaa kwa kuwa wazazi nao walitumia muda mwingi kuwahudumia, zaidi ameitaka jamii na wadau kushirikaina kwa pamoja kuwajali na kuwahudumia wazee.
"Wazee wanahitaji upendo, wanahitaji kulelewa na kuthaminiwa, tusiwatelekeze na kuona hawafai bali tushirikiane kuwahudumia na sio kuiachia serikali peke yake, kwa kufanya hivyo watapata baraka kutoka kwa Mwenyenzi Mungu, tutambue kuwa wazee hawa ni tunu ya taifa letu, tunalo jukumu la kuwabudumia bila kuchoka" Asisitiza Mhe. Dkt. Ojung'u
Naye Afisha Ustawi wa Jamii, halmashauri ya Arusha Beatrice Tengi amesema kuwa ugawaji wa chakula hicho umezingatia wazee wenye uhitaji zaidi na kufafanua kuwa kila mmoja amepata Kilo 10 za mchele, chumvi sukari na sabuni za kufulia.
Awali Maadhimisho ya Siku ya Wazee yana lenga kuhamasisha jamii kuongeza uelewa wa juu ya masuala yanayohusu uzee na kuzeeka ikiwemo haki zao na upatikanaji wa huduma muhimu kwa wakati.
Kauli mbiu:"Udhibiti wa Wazee kwenye Dunia yenye mabadiliko"
ARUSHA DC NI YETU, TUSHIRIKIANE KUIJENGA
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.