• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WILFRED DANIEL AWA MWENYEKITI MWENZA WA BARAZA LA BIASHARA WILAYA YA ARUMERU.

Posted on: November 19th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Mfanyabiashara Wilfred Daniel amechakuguliwa kuwa Mwenyekiti Mwenza wa Baraza la Wafanya biashara wilaya ya Arumeru baada ya kushinda kwenye uchaguzi uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmasahuri ya Meru, Baraza linalojumuisha halmashauri za Arusha na Meru zinazounda wilaya ya Arumeru.

Mfanya biashara huyo amepata nafasi hiyo, na kupewa dhamana ya kuliongoza Baraza hilo kwa kipindi cha miaka 3, kwa kupata kura 19 kati ya kura 49 zilizopigwa na kuwashinda wagombea wenzake watatu waliowania nafasi hiyo.

Awali Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyabiashara wilaya ya Arumeru ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango, kwa mujibu wa Kanuni, amemtangaza Mfanyabiashara Wilfred Daniel kuwa Mwenyekiti mwenza wa Baraza hilo, huku akimtangaza Makamu Mwenyekiti Mwenza CPA. Maija Mchau aliyepata kura 17.

Aidha Mhandisi Ruyango, amewataka viongozi hao kusimamia miongozo na kuyafahamu madhumuni ya Baraza ili kuweka mkakati wa utekelezaji na kuyafikia malengo ya baraza kwa kushirikishana kutatua changamoto zinazowakabili wafanyabiashara kwa maendeleo ya wananchi na Taifa.

"Serikali inatambua huduma mnayoitoa kwa jamii, ninawaagiza viongozi, kaeni na wafanyabiashara wenzenu mpate maoni yao, ili kuishauri serikali namna bora ya kuenenda ili kuwa na mazingira rafiki ya kuendesha  biashara, yanayochochea maendeleo binafsi na ya Taifa". Amesisitiza mkuu huyo wa wilaya

Hata hivyo baada ya uchaguzi huo, Mwenyekiti mwenza licha ya kuwashukuru wajumbe kwa kumuamini na kumpa nafasi hiyo , ameahidi kushirikiana na wafanyabiashara wote kwa kuitumikia nafasi hiyo kwa uaminifu ili kufikia lengo la serikali kupitia Baraza la wafanayabishara la kuwaunganisha na serikali.

Mkuu wa Idara ya Biashara na Uwekezaji, halmashauri ya Meru, Noel Pallangyo ameyataja madhumuni ya Baraza la Biashara la wilaya ni kuwakutanisha Sekta Binafsi na Serikali ili kujadili na kupeana ushauri wa namna ya kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji katika Wilaya na kukuza sekata ya uchumi.

Majukumu mengine ni pamoja na kutengeneza mazingira bora ya kufanyia Biashara na uwekezaji, Kuibua fursa za uwekezaji, kuzinadi fursa hizo kupitia makongano mbalimbali pamoja na kufanya matangazo ya biashara.

Baraza la Taifa la Biashara la wilaya lilianzishwa chini mwaka 2001 kwa waraka wa Rais na 1 wa mwaka 2001 ukielekeza kila wilaya liunde Baraza la Biashara la Wilaya ikiwa ni jitihada ya kukuza uchumi ndaninya wilaya, wilaya ya Arumeru imeunda Baraza hilo na kuchagua viongozi watakaoongoza kwa miaka miatatu.


Mwenyekiti Mwenza wa Baraza la Biashara wilaya ya Arumeru, Wilfred Daniel, akizungumza na wajumbe wa Baraza hilo mara baada ya kutangazwa mshindi na kushika nafasi hiyo kwa miaka mitatu.

Makamu Mwenyekiti Mwenza wa Baraza la Biashara wilaya ya Arumeru, CPA. Maija Mchau akizungumza na wajumbe wa Baraza hilo mara baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo kwa miaka mitatu.

Mkuu wa wilaya ya Arumeru na Mwenyekiti wa Baraza la Biashara wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango, akiongoza mkutano wa robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2022/2023, uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Meru


Baadhi ya wafanyabiashara waliohudhuria mkutano wa Baraza la Biashara wilaya ya Arumeru uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Meru

Baadhi ya wafanyabiashara waliohudhuria mkutano wa Baraza la Biashara wilaya ya Arumeru uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Meru

Wakuu wa Idara na Vitengo, halmashauri ya Arusha wakiwa kwenye mkutano wa Baraza la Biashara wilaya ya Arumeru uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Meru


Wakuu wa Idara na Vitengo, halmashauri ya Arusha wakiwa kwenye mkutano wa Baraza la Biashara wilaya ya Arumeru uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano halmashauri ya Meru




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.