Na Elinipa Lupembe
Wananchi wa kijiji cha Bwawani kitongoji cha Olmapinuu, wakifanyakazi ya kuwasaidia mafundi kujenga nyumba ya mwalimu, kwenye shule shikizi Olokii, ujenzi unaotekelezwa na serikali kwa gharama ya shilingi milioni 50 fedha kutoka Serikali Kuu.
Wananchi hao, wamebainisha kufikia hatua hiyo, kutokana na kuona umuhimu wa nyumba hiyo ya mwalimu shuleni hapo, nyumba ambayo walimu wataishi hapo na kuwafundisha watoto wao kwa amani na utulivu.
Mjumbe wa kamati ya Mapokezi ya Ujenzi, Shaban Rashid amesema kuwa, watoto wao wamekuwa wakiteseka kwa miaka mingi, kutokana na shule ya msingi kuwa mbali na kutenganishwa na korongo ambalo wakati wa mvua watoto hushindwa kuvuka na kukosa masomo kwa zaidi ya miezi 4 mpaka 6 wakati mwingine.
"Tunamshukuru mama Samia, kweli amekikumbuka kijiji chetu hasa kitongoji cha Olmapinuu, kitongoji ambacho watoto wengi waliacha shule kwa kukata tamaa ya umbali na wengine kucheleweshwa kuandikishwa shule kutokana na wazazi kuhofia madhara watakayokutana nanyo njiani hasa kipindi cha mvua". Amefafanua Ally.
Aidha ameipongeza serikali kwa kuwashirikisha wananchi katika usimamizi wa miradi, jambo ambalo linawafanya wananchi, kumiliki miradi lakini linawafanya kujihakikishia matumizi sahihi ya pesa zao za Umma.
Awali Serikali inandelea na mkakati wa kuboresha miundo mbinu ya shule ili kuhakikisha watoto wenye umri wa kwenda shule, wanaandikishwa kwa wakati.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍
PICHA ZA WANANCHI WAKISHIRIKI UJENZI WA NYUMBA YA MWALIMU
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.