# Wanawake wameonesha kuwa chachu ya uanzishwaji wa viwanda vidogo kwa kuwa mpaka sasa asilimia 60% ya viwanda vidogo vinamilikiwa na wanawake.
# Wanawake wametakiwa kujikita kwenye uzalishaji wa malighafi na bidhaa za viwanda, vitakavyowawezesha kujiajiri na kuajiri katika kuelekea uchumi wa kati na uchumi wa viwanda.
# Halmashauri imejipanga kuwainua na kuwajengea uwezo wanawake wajasiriamali wanaojihusisha na usindikaji ili kuinua viwanda hivyo kuelekea viwanda vya kati hadi vikubwa. # Halmashauri imejipanga kukusanya mapato ya ndani kwa lengo la kupata asilimia 4% ya kuwakopesha wanawake, na kuwataka wanawake hao kulipa kodi na ushuru wa bidhaa zao ili kuwezesha halmashauri kupata mapato.
# Halmashauri imewafikiwa jumla ya wananwake 605 kwenye vikundi 54 kwa kuwapatia mikopo yenye tahamani ya shilingi milioni 290 na kufikisha kiasi cha shinigi milioni 600 kukopeshwa kwa vikundi vya wananwake tangu halamshauri ilipoanz amwaka 2007.
# Idara ya Maendeleo ya Jamii imetakiwa kuwanganisha Wanawake wajasiriamali ili bidhaa zao ziweze kusajiliwa na kupata vibali vya viwango vitakavyowezesha bidhaa zao kupata soko ndani na nje ya Tanzania.
# Halmashauri imejikita katika kutatua changamoto za wanawake ikiwemo kuboresha hali za uchumi kwa kutoa mikopo, kuboresha sekta za elimu kwa kuhakikisha watoto wa kike wanapata elimu, kuboresha miundo mbinu ya huduma za afya kwa lengo la kupunguza vifo vya mama na mtoto, kuboresha huduma za maji kwa kutekeleza miradi mingi ya maji ili kumpunguzia mama mzigo wa kuchota maji na kutekeleza kampeni ya kumtua mama ndoo.
# Viongozi wamekiri kupambana na mila kandaamizi dhidi ya wanawake na kuthibitisha kuwa ukeketaji wa watoto wa kike umepungua kwa kiasi kikubwa na zaidi unaelekea kwisha kabisa, viongozi wako tayari kulinda na kutetea masilahi ya wanawake ili kuwa na taifa lenye nguvu na kujiamini.
# Dunia inatambua changamoto zinazowakabili wanawake zinazotokana na wanaume kukwepa majukumu, lakini Mungu anasikia kilio cha wanawake na kutambua kuwa wanawake ni jeshi kubwa na lenye ushawishi, hivyo wanatakiwa kuungana na kufanya ushawishi wa maendeleo ya taifa la Tanzania. # Wanawake wametakiwa kuwa na nidhamu ya mikopo pamoja na kujenga tabia ya kujiweke akiba benki jambo ambalo litawawezesha kupata mikopo mikubwa zaidi pindi biashara zao zitakapokuwa kubwa.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.