Na. Elinipa Lupembe.
# Kwa baadhi ya kata ambazo hazina shule za sekondari, halmashauri, madiwani kwa kushirikiana wananchi kutafuta maeneo ya kijenga shule, na kutokana na uhaba wa ardhi katika maeneo hayo, kutekeleza ujenzi wa majengo ya ghorofa ili kumeneji matumizi bora ya ardhi.
# Kutokana na ongezeko la wanafunzi wanaoandikishwa tangu serikali kutoa elimu bila malipo, halmashauri imejipanga kuendelea na maandalizi ya uejnzi wa vyumba vya madarasa unaoendana na maoteo sahihi yatakayotokana na sensa ya wanafunzi itakayofanyika mapema mwezi Aprili 2021.
# Viongozi wawakilishi wa wananchi wanajukumu kubwa la kuhamasisha wazazi kuchangia chakula kwa watoto wao kwa shule za msingi na shule za kutwa za sekondari ili kuahkikiaha wanafunzi wotw wanapata chakula wawapo ahuleni.
# Uongozi wa halamshauri unaenselea kusimamaia watumishi wote kutekeleza majukumu yao kisekta, ili kuahkikisha wananchi wa halmashauri ya Aruaha wanapata huduma zote muhimu zinazotolewa na serikali yao.
# Licha ya kuwa katika kata zote kuna changamoto katika sekta ya afya, elimu, kilimo, mifugo, maji na miunsombinu ya barabara, bado serikali ya awamu ya tano inaendelea kutatua changamoto hizo kisekta kwa kuzingatia vipaumbele na mpango wa bajeti na uapatikanaji wa fedha kwa mwaka.
# Halmashauri inawataka wananchi na wadau wa maendeleo kujitokeza kwa wingi kishiriki katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo lengo likiwa ni kutatua changamoto za kijamii kwa wananchi wote waweze kupata husuma bora katika maeneo yao.
# Kuendelea kuimarisha mipango ya kusimamia vyanzo vya mapato na ukusanyaji wa mapato, pamoja na kubuni vyanzo endelevu vya mapato vitakavyowezesha kuendesha miradi ya maendeleo ya kuwahudumia wananchi wetu, kuanzia ngazi ya kijiji mpaka ngazi ya halmashauri.
# Ofisi ya Mkurugenzi kwa kishirikiana na ofisi ya mkuu wa wilaya, inaendelea kushughulikia migogoro ya muda mrefu ya mipaka kati ya Halmashauri ya Meru kata ya Bangata na Kata ya Olsonyowas na mgogoro kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Longido, ili kuahakikisha wanachi wanafanya shughuli zao kwa amani na utulivu.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Arusha, Mheshimiwa Ojung Salekwa akizungumza wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la kuwasilsiha Taarifa za Kata kwa kipindi cha robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2020/2021.
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, Saad Mtambule, akizungumza wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la kuwasilsiha Taarifa za Kata kwa kipindi cha robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2020/2021.
Diwani wa Kata ya Olturoto, Mheshimiwa Baraka Simon akiwasilsiha Taarifa za Kata ya Olturoto kwa kipindi cha robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2020/2021 kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani la kuwasilsiha Taarifa za Kata za robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2020/2021.
Diwani wa Kata ya Kimnyaki, Mheshimiwa Eliakimu Mervey, akiwasilsiha Taarifa za Kata ya Olturoto kwa kipindi cha robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2020/2021 kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani la kuwasilsiha Taarifa za Kata za robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2020/2021.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.