Na. Elinipa Lupembe.
*Idara ya Mazingira kufanya tathmini ya athari za uharibifu wa mazingira katika mlima Kivesi, zinazodaiwa kutokana na uwekaji minara ya simu katika milima huo.
**Idara ya Fedha na Biashara, ifanye tathmini na kuwabaini wafanyabiashara wote, wanaotumia Vitambulisho vya Machinga huku hawana sifa hizo, na kuvitumia kama kivuli cha kutokulipa kodi ya Serikali, watakaobainika wachukuliwe hatua za kisheria, ikiwa ni pamoja na kushtakiwa kwa kukwepa kulipa kodi na kuingizia Serikali hasara
***Wamesisitiza, Idara hiyo ya Fedha kufuata sifa za wafanyabiashara zilizoainishwa na Mhe. Rais, Dkt. John Magufuli, vitambulisho vya Machinga ni kwa ajili ya mfanyabiashara mwenye mtaji usiozidi shilingi milioni 4, na sio vinginevyo.
******Menejimenti iongeze nguvu kwenye kikosi kazi cha Ukusanyaji Mapato ya Halmashauri, kwa kuwashirikisha Maafisa Watendaji wa Kata na Vijiji ili kuongeza kasi na guvu ya ukusanyaji katika maeneo yao.
*****Idara ya Sheria kuanza mchakato wa sheria ndogo za halmashauri, zitakazowezesha Vijiji na Halmashauri kunufaika na minara iliyopo katika maeneo yao.
******Wananchi wanatakiwa kuwasilisha changamoto zote zinazojitokeza wakati wa zoezi la Urasimishaji wa Makazi unaendelea, katika maeneo mbalimbali, kwenye Ofisi ya Ardhi, Kitengo cha Mipango Miji, halmashauri ya Arusha licha ya kuwa Kazi hizo zinafanywa na Kampuni binafsi ambazo zimepewa Kandarasi hiyo na Serikali.
*******Vikao vya Kisheria vifanyike kwa wakati, ili kupata nafasi ya tathmini utekelezaji wa shughuli za maendeleo na kuweka mipango thabiti inayoendana na muda wa bajeti kwa kipindi husika.
********Manajimenti ifanye ufuatiliaji wa deni la fidia ya shamba la Lakilaki, ambalo halmashauri inazidai kutoka Serikali Kuu kiasi cha shilingi bilioni 1.9, ili fedha hizo ziweze kulipwa na kutekeleza miradi ya halmashauri.
********Halmashauri itoe fedha kwa ajili ya miradi mingi inayotekelezwa kwa nguvu za wananchi, ili kuwatia moyo wananchi wanaojitoa kwa hali na mali kujenga nchi yao.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.